Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 8 | Energy and Minerals | Wizara ya Nishat | 87 | 2026-04-14 |
Name
Kenneth Ernest Nollo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bahi
Primary Question
MHE. ESTER A. BULAYA K.n.y. MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza kusafisha mafuta ghafi yanayotoka Uganda kupitia Bomba la Mafuta EACOP?
Name
Salome Wyckiffe Makamba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, ninaomba kujibu swali namba 87 la Mheshimiwa Kenneth Ernest Nollo, Mbunge wa Bahi, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, ushiriki wa Tanzania kwenye mradi wa bomba la EACOP upo kwenye biashara ya kusafirisha mafuta ghafi tu, yaani transit nation kutoka Kabaale – Hoima hadi Chongoleani – Tanga na baadaye kupelekwa kwenye masoko ya Kimataifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mikataba ya mauzo ya mafuta hayo imeshaingiwa tayari kati ya wabia wa mkondo wa juu nchini Uganda, yaani up streamers ambao ni Serikali ya Uganda na makampuni ya Kimataifa ya Total Energies kutoka Ufaransa na CNOOC kutoka China kwa kuzingatia vigezo vya usanifu wa kitaalamu na uwezo wa uzalishaji wa visima.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba ifahamike kwamba kwenye biashara hii tayari mikataba ya mauzo ya mafuta haya imeshaingiwa kati ya wabia wa mkondo wa juu na wanunuzi wa masoko ya Kimataifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuwasilisha.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved