Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 8 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 87 2026-04-14

Name

Kenneth Ernest Nollo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. ESTER A. BULAYA K.n.y. MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza kusafisha mafuta ghafi yanayotoka Uganda kupitia Bomba la Mafuta EACOP?

Name

Salome Wyckiffe Makamba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer


NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, ninaomba kujibu swali namba 87 la Mheshimiwa Kenneth Ernest Nollo, Mbunge wa Bahi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushiriki wa Tanzania kwenye mradi wa bomba la EACOP upo kwenye biashara ya kusafirisha mafuta ghafi tu, yaani transit nation kutoka Kabaale – Hoima hadi Chongoleani – Tanga na baadaye kupelekwa kwenye masoko ya Kimataifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mikataba ya mauzo ya mafuta hayo imeshaingiwa tayari kati ya wabia wa mkondo wa juu nchini Uganda, yaani up streamers ambao ni Serikali ya Uganda na makampuni ya Kimataifa ya Total Energies kutoka Ufaransa na CNOOC kutoka China kwa kuzingatia vigezo vya usanifu wa kitaalamu na uwezo wa uzalishaji wa visima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba ifahamike kwamba kwenye biashara hii tayari mikataba ya mauzo ya mafuta haya imeshaingiwa kati ya wabia wa mkondo wa juu na wanunuzi wa masoko ya Kimataifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuwasilisha.