Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mgore Miraji Kigera

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Musoma Mjini

Primary Question

MHE. MGORE M. KIGERA aliuliza: - Je, upi mkakati wa Serikali wa kuhakikisha mwekezaji wa Kiwanda cha MUTEX anaanza uzalishaji kwa haraka?

Supplementary Question 1

MHE. MGORE M. KIGERA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ninashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Je, Serikali haioni wakati sahihi umefika kuhakikisha wanakamilisha makubaliano na kusaini mkataba na mwekezaji huyo ili kuweza kutekeleza ahadi yake kwa wananchi wa Jimbo la Musoma Mjini, kukuza ajira na uchumi wa Musoma Mjini kupitia kiwanda hiki cha MUTEX?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Ni lini Serikali itawalipa waliokuwa wafanyakazi wa kiwanda hicho cha MUTEX kwani tangu mwaka 1994, wafanyakazi hao wamekuwa wakiidai Serikali fedha zao? Ninashukuru. (Makofi)

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MIPANGO NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ninachukua nafasi hii kumshukuru na kumpongeza sana Mheshimiwa Mgore Miraji Kigera, Mbunge wa Jimbo la Musoma Mjini, kwa kuendelea kufuatilia kwa ukaribu sana kuhusu hiki Kiwanda cha MUTEX ambacho kimsingi, kama kitafufuliwa, kitakuwa na tija sana kwa wananchi wa Musoma Mjini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme, Mheshimiwa Mbunge amekuwa akitusumbua sana na amefuatilia kwa karibu sana kuhusu hiki kiwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya maneno hayo, ninaomba kujibu maswali mawili yaliyoulizwa na Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nia na dhamira ya Serikali ni kuhakikisha kwamba tunavutia wawekezaji, na sisi kama Serikali tumejipanga, maeneo yote yale ambayo kimsingi yapo idle, hayafanyi kazi, tunatafuta wawekezaji ili tuweze kuhakikisha tunawekeza. Hii ni sehemu ya utekelezaji wa Dira yetu ya 2050.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuzingatia hilo, na sisi tumeona kuna haja sasa ya ku-fast track process ya kuhakikisha kwamba huyu mwekezaji anasaini mkataba kwa haraka. Pia tutamsimamia, tutampa performance contract, ili ndani ya muda mfupi tuone uwekezaji unaanza katika Jimbo la Musoma Mjini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vigezo vikubwa ambavyo tunaviweka kwa sasa hivi, kwanza tunataka mwekezaji atakaposaini mkataba, atoe commitment, ni lini ataanza kuwekeza katika eneo la Musoma Mjini? Pili, ni kiasi gani cha ajira atakuja kuzalisha? Tatu, tunataka achangie katika mnyororo wa thamani, hususan katika Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Ni kweli kulikuwa kuna wafanyakazi ambao walikuwa wanafanya kazi katika kiwanda cha MUTEX, takribani 935. Kati ya hao, wafanyakazi 856 walishalipwa mafao yao na wafanyakazi 79 walikuwa bado hawajalipwa mafao yao. Hawa 79 hawakujitokeza wakati wa uhakiki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachukua nafasi hii sasa kuwataka wale wote 79 ambao hawakujitokeza, wakati tunafanya uhakiki, wapeleke nyaraka zao kwenye ofisi ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, wahakikiwe na baada ya kuhakikiwa Serikali itakuwa tayari kuwalipa. Ahsante.

Name

Christina Solomon Mndeme

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MGORE M. KIGERA aliuliza: - Je, upi mkakati wa Serikali wa kuhakikisha mwekezaji wa Kiwanda cha MUTEX anaanza uzalishaji kwa haraka?

Supplementary Question 2

MHE. CHRISTINA S. MNDEME: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa, Serikali imekuwa ikifanya kazi nzuri ya kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji nchini, na kwa kuwa kiwanda cha nyuzi cha Tabora, (TABOTEX) kimesimama miaka mingi sana bila kufanya kazi, je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba kiwanda hiki cha nyuzi Tabora kinafufuliwa na kuanza kufanya kazi ili kiweze kutoa ajira kwa Wanatabora na Watanzania kwa ujumla na kukuza uchumi?

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MIPANGO NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ninachukua nafasi hii kumshukuru na kumpongeza sana Mheshimiwa Mbunge kutoka Mkoa wa Tabora. Ninajua michango yake mingi nimekuwa nikiifuatilia, amekuwa akichangia sana kwenye suala la uwekezaji, na jinsi ya kuwezesha kinamama katika suala la uchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli hiki kiwanda cha nyuzi cha Tabora ambacho kimesimama kama tutakifufua kitakuwa na tija sana kwa uchumi wa Taifa. Ninaomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba sisi kama Serikali tumeweka mkakati wa kutathmini viwanda vyote ambavyo vimesimama na baada ya tathmini hiyo tutaandaa mpango mkakati wa kuvifufua ikiwa ni pamoja na kuvutia wawekezaji. Ahsante sana.

Name

Paschal Inyasi Chinyele

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Primary Question

MHE. MGORE M. KIGERA aliuliza: - Je, upi mkakati wa Serikali wa kuhakikisha mwekezaji wa Kiwanda cha MUTEX anaanza uzalishaji kwa haraka?

Supplementary Question 3

MHE. PASCHAL I. CHINYELE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kumwuliza Mheshimiwa Naibu Waziri, ni lini Serikali itatekeleza mpango wa ujenzi wa viwanda katika kongani za viwanda katika kata za Nala pamoja na Mpunguzi?

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MIPANGO NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachukua nafasi hii kwanza kumpongeza Mheshimiwa Chinyele, Mbunge wa Dodoma Mjini, kwa kuwatetea wananchi wa Dodoma, hususan wananchi wa Nala na wananchi wa Mpunguzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye mpango wetu wa miaka minne, tume-commit kuanzisha miradi saba ya kielelezo (National Flagship Programs). Katika ile miradi saba ya kielelezo, tunakuja kuanzisha kongani ya viwanda eneo la Nala ambayo kimsingi tunaweka pale viwanda vya kuchenjua dhahabu kwenye madini ambayo ni rare na critical, kwa mfano lithium, cobalt, nickel na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa eneo la Mpunguzi tumelitenga kama eneo la mkakati kwa sababu Mpunguzi wanazalisha sana zabibu. Kwa hiyo, ninamwondoa mashaka Mheshimiwa Chinyele, Mbunge wa Dodoma Mjini, kwamba hili lipo kwenye mpango wetu wa miaka mitano. Pia, tumeliingiza na kwenye mpango wa mwaka mmoja, tumelitengea bajeti. Ninashukuru. (Makofi)