Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cornel Lucas Magembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato Kaskazini

Primary Question

MHE. CORNEL L. MAGEMBE aliuliza: - Je, lini Serikali itatoa fedha za ujenzi wa Kituo cha Afya Nyamirembe ambapo ni Makao Makuu ya Tarafa?

Supplementary Question 1

MHE. CORNEL L. MAGEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, ninayo maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, ninapenda kujua Mheshimiwa Naibu Waziri ni lini atapanga safari ya kwenda na mimi jimboni ili akajionee hali halisi ya Kata ya Nyamirembe ambayo ni makao makuu ya tarafa ambayo ina wakazi zaidi ya 23,000 na vijiji vinne ambao wanahitaji kwa haraka utekelezaji wa ujenzi wa kituo hiki cha afya?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa vile tayari Serikali imeshapeleka fedha za kukamilisha ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kasenga, lakini Kasenga ni moja ya kata zilizoko kwenye Tarafa ya Kachwamba, ambapo kuna kata nne ambazo mpaka sasa hawana gari la wagonjwa (ambulance). Je, Serikali ina mpango gani katika kuhakikisha kwamba wananchi hao wanapata ambulance ambayo itawasaidia katika kuwaharakisha kuwapeleka katika hospitali nyingine?

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kujibu maswali mawili madogo ya nyongeza ya kaka yangu Mheshimiwa Cornel Lucas Magembe, kule tumezoea kumwita mwalimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ninampongeza sana Mheshimiwa Magembe kwa kuendelea kuwapambania Wananchi wa Jimbo la Chato Kaskazini. Nianze kwa kujibu swali la kwanza kwamba lini tutafanya ziara katika kata hii yenye wakazi zaidi ya 23,000 ili kujionea hali halisi na kuboresha miundombinu? Nimwambie tu kaka yangu, kwamba Jimbo la Chato Kaskazini liko katika Mkoa wa Geita, na mimi ninatokea Mkoa wa Geita, Jimbo la Busanda. Kwa hiyo, huyu ni jirani yangu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tutatenga muda mimi na yeye tuweze kwenda kuwaona wananchi hao na kuwaambia nini Serikali inaendelea kufanya kwa ajili ya maendeleo yao?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari tumeshawasiliana na wenzetu Wizara ya Afya, zile ambulance ambazo zimeshafika tuweze kuzitoa na tumalizie taratibu za Kiserikali ili tuweze kuwapatia hasa wahitaji, na hasa zile kata ambazo hazikupata na zile halmashauri ambazo hazikupata waweze kupata ambulance hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuwasilisha.

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. CORNEL L. MAGEMBE aliuliza: - Je, lini Serikali itatoa fedha za ujenzi wa Kituo cha Afya Nyamirembe ambapo ni Makao Makuu ya Tarafa?

Supplementary Question 2

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nimekuwa nikisimama mara kadhaa hapa kuomba ujenzi wa Kituo cha Afya Matamba, kituo ambacho kinahudumia takribani kata tano. Kituo hiki kina hali mbaya sana, hakipo kabisa kwa maana ni cha mwaka 1970. Je, ni lini watajenga kituo kipya cha afya kama ambavyo wameahidi kwenye hotuba zao mara kadhaa?

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sanga. Kwanza, tulifanya ziara katika Halmashauri ya Wilaya ya Makete. Ninampongeza tu kwamba, wananchi wa kule ni waungwana sana, walitupokea walitupa na wawadi. Japokuwa kuna miinuko na milima ya hatari, lakini tuliweza kufika tukafanya ziara nzuri tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Sanga, kituo hiki cha afya cha kimkakati tayari pamoja na yale majimbo mengine ambayo bado hayajapata, tumeshapeleka andiko Hazina, na tayari Hazina wameshapitisha andiko letu. Kwa hiyo, fedha zikiingia tutakwenda kukamilisha ujenzi wa kituo hiki cha kimkakati.

Name

Joseph Enock Tama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kaliua

Primary Question

MHE. CORNEL L. MAGEMBE aliuliza: - Je, lini Serikali itatoa fedha za ujenzi wa Kituo cha Afya Nyamirembe ambapo ni Makao Makuu ya Tarafa?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH E. TAMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itatoa fedha za ujenzi wa Kituo cha Afya cha Igwisi katika Jimbo la Kaliua?

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Kaliua kwamba pamoja na yeye tayari tumeshawasilisha andiko kuhusu hili ombi la fedha kutoka Hazina. Kwa hiyo, kituo cha afya cha kimkakati katika Jimbo la Kaliua, kwa confidence kabisa nimwambie Mheshimiwa Mbunge awaambie wananchi kwamba tunakwenda kukijenga na kianze kutoa huduma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuwasilisha.

Name

Jonas William Mbunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. CORNEL L. MAGEMBE aliuliza: - Je, lini Serikali itatoa fedha za ujenzi wa Kituo cha Afya Nyamirembe ambapo ni Makao Makuu ya Tarafa?

Supplementary Question 4

MHE. JONAS W. MBUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Serikali ilitoa shilingi milioni 250 kwa ajili ya kujenga kituo cha afya kilichopo Kata ya Myangayanga katika Jimbo la Mbinga Mjini, lakini yalijengwa majengo mawili: jengo la OPD pamoja na jengo la maabara. Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa Kituo cha Afya cha Myangayanga?

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuwa Serikali ilitoa fedha za kujenga vituo vya afya hivi, kwa kuanzia na shilingi milioni 250 katika maeneo yote nchini. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, na nimwelekeze Mkurugenzi kwa niaba ya Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI kuendelea kutenga fedha ili kukamilisha miundombinu katika hospitali zetu hizi hizi ili kuendelea kutoa huduma katika vituo vyote vya afya.

Name

Ado Shaibu Ado

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. CORNEL L. MAGEMBE aliuliza: - Je, lini Serikali itatoa fedha za ujenzi wa Kituo cha Afya Nyamirembe ambapo ni Makao Makuu ya Tarafa?

Supplementary Question 5

MHE. ADO S. ADO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Jimbo la Tunduru Kaskazini ni moja kati ya majimbo ambayo hayana kituo cha afya kwa kila tarafa, na kwa kuwa Tarafa ya Nampungu ni tarafa pekee ambayo haina kituo cha afya na haijapata bajeti ya kutosha katika ukamilishaji wa ujenzi wa kituo hicho cha afya, je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Kituo cha Afya Mpungu?

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba pia Jimbo la Tunduru Kaskazini lipo katika mpango wa kupata kituo cha afya cha kimkakati; na kwenye yale maombi tuliyowasilisha Hazina kimo kituo hiki cha afya cha Mheshimiwa Mbunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tutaendelea kukamilisha baadhi ya majengo katika vituo vya afya ambavyo bado havijakamilika ili kuendelea kutoa huduma kwa watu wetu wa Jimbo la Tunduru kaskazini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuwasilisha.