Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 8 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) | 74 | 2026-04-14 |
Name
Cornel Lucas Magembe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Chato Kaskazini
Primary Question
MHE. CORNEL L. MAGEMBE aliuliza: -
Je, lini Serikali itatoa fedha za ujenzi wa Kituo cha Afya Nyamirembe ambapo ni Makao Makuu ya Tarafa?
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF) alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Cornel Lucas Magembe, Mbunge wa Jimbo la Chato Kaskazini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi cha mwaka wa fedha 2021/2022 hadi mwaka 2025/2026 Serikali imejenga na kuboresha jumla ya vituo vya afya vitano katika Halmashauri ya Wilaya ya Chato kwa gharama ya jumla shilingi bilioni 2.64.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi cha mwaka wa fedha 2024/2025 na mwaka 2025/2026 Serikali imetoa jumla shilingi milioni 489 kwa ajili ya uboreshaji wa miundombinu katika zahanati ya Kasenga na kuwa kituo cha afya chenye uwezo wa kutoa huduma za dharura na za upasuaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2026/2027 Serikali imetenga jumla shilingi milioni 300 kwa ajili ya ukamilishaji wa vituo vya afya katika Halmashauri ya Wilaya ya Chato kikiwemo Kituo cha Afya Iparamasa kilichotengewa jumla shilingi milioni 108.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya kwenye kata za kimkakati kikiwemo Kituo cha Afya Nyamirembe ili kusogeza huduma za dharura na upasuaji kwa mama wajawazito.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuwasilisha.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved