Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Jonas William Mbunda
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mbinga Mjini
Primary Question
MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga minara ya simu katika Kata za Kikolo na Kagugu?
Supplementary Question 1
MHE. JONAS W. MBUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ninaipongeza Serikali kwa majibu mazuri. Pili ninaishukuru Serikali kwa kuanza kujenga mnara wa simu katika Kata ya Kikolo, na pia kufikiria kuanza kufanya tathmini ya kujenga mnara wa simu katika Kata ya Kagugu. Nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, mradi unaoanza kutekelezwa kujengwa mnara katika Kata ya Kikolo unakwenda kwa kusuasua. Nataka nijue, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa mnara huo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Kijiji cha Ruangai eneo la Kipungu Kata ya Mpepai kuna changamoto kubwa ya mawasiliano ya simu. Ni lini Serikali itaweka mkakati wa kuhakikisha kwamba inajenga mnara wa simu katika eneo hili ili wananchi waweze kupata mawasiliano?
Name
Switbert Zacharia Mkama
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ukerewe
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ujenzi wa mnara tulioutaja katika Kijiji cha Kikolo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kazi hii itakamilika tarehe 30 Juni, 2026, kwa sababu tayari mkandarasi ameshapatikana na anaendelea na mobilization. Atakapokamilisha mobilization, ujenzi utaanza mara moja. Ifikapo tarehe 30 mwezi wa Sita, ujenzi huu utakamilika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu changamoto ya mawasiliano katika Kijiji cha Luhangali, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika mkakati wetu wa Serikali wa miaka mitano kuanzia mwaka 2025 kwenda mwaka 2030, tutafanya tathmini katika maeneo yote yenye changamoto na tutayafikia. Tutaanza na maeneo ya changamoto kubwa, changamoto za kati na changamoto zenye unafuu. Kwa hiyo, tutapitia zote na kuhakikisha kwamba ifikapo mwaka 2030 kila Mwananchi wa Tanzania atakuwa na uso wenye furaha katika sekta hii ya mawasiliano.
Name
Happiness Daniel Ngwando
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga minara ya simu katika Kata za Kikolo na Kagugu?
Supplementary Question 2
MHE. HAPPINESS D. NGWANDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kuuliza swali la nyongeza. Serikali ina mpango gani wa kuweka network kwenye hospitali zetu ambazo zinatumia system, ili kupunguza mgonjwa kukaa muda mrefu kumsubiria daktari apate network. Kwa mfano, Hospitali ya Wilaya ya Nyasa na Nangombo, Tunduru, ili daktari apate network inabidi atoke nje kutafuta mnara. Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka network haraka ili wananchi wetu wasipate usumbufu wa kusubiri majibu muda mrefu hususan wanawake wa Mkoa wa Ruvuma? Ahsante.
Name
Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Nominated
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyoeleza kwamba tuna mkakati wa miaka mitano wa kupeleka mawasiliano ya simu na data katika maeneo yote nchini. Katika haya maeneo ya hospitali na maeneo mengine muhimu, tutayatekeleza katika awamu ya 11 ambapo Serikali ina mpango wa kupeleka mawasiliano ya internet na data katika maeneo ya mkakati yakiwemo haya ya miundombinu ya Serikali ikiwemo Reli ya TAZARA, SGR, MGR ikiwemo mbuga ya hifadhi za wanyama na maeneo mengine ya kimkakati kama hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba eneo hilo pia kama Serikali tunalifanyia kazi na lipo kwenye mkakati mahususi wa Wizara. Kwa hiyo, tutalifanyia kazi na maeneo yote hayo yatapata mawasiliano ya internet.
MWENYEKITI: Mheshimiwa Waziri.
WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri na tumshukuru sana Mheshimiwa Happiness kwa maswali yake na kuweka msisitizo kuhakikisha kwamba Wilaya ya Nyasa na Tunduru zinapata mawasiliano ya uhakika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Happiness, katika mradi wetu wa utekelezaji wa ujenzi wa minara 201, Wilaya ya Nyasa tutaweka minara miwili katika Kata ya Liuli pamoja na Mpepo. Vilevile kwa Wilaya ya Tunduru tutajenga mnara katika Kata ya Mchesi pamoja na Mlingoti Magharibi. Hivyo basi, niendelee kumhakikishia kwamba sasa hivi tunakamisha ujenzi wa minara 908 katika kata 730, na tutahakikisha kama Mheshimiwa Naibu Waziri alivyoeleza katika makakati wetu, tuwahakikishie Waheshimiwa Wabunge, ifikapo 2030 hakuna eneo ambalo litakuwa halina mawasiliano. Nashukuru kwa nafasi. (Makofi)
Name
Lucy Edward Mwakyembe
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga minara ya simu katika Kata za Kikolo na Kagugu?
Supplementary Question 3
MHE. LUCY E. MWAKYEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali katika Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari. Ni utaratibu gani unaotumika kwa kutumia mkongo wa Taifa katika kupeleka mawasiliano kule Zanzibar ili kufikisha huduma kwa wateja kwa haraka sana na kwa maeneo ambayo hayafikiki?
Name
Switbert Zacharia Mkama
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ukerewe
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, utaratibu unaotumika katika kupeleka mawasiliano Zanzibar kupitia mkongo wa Taifa, huwa kwanza inafanyika tathmini, kuangalia uhitaji wa maeneo husika, ikishafanyika, Shirika la Mawasiliano Nchini hupeleka mawasiliano hayo kulingana na uhitaji wa eneo husika.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved