Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 7 | Information, Communication and Information Technology | Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari | 69 | 2026-04-13 |
Name
Jonas William Mbunda
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mbinga Mjini
Primary Question
MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza:-
Je, lini Serikali itajenga minara ya simu katika Kata za Kikolo na Kagugu?
Name
Switbert Zacharia Mkama
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ukerewe
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jonas William Mbunda, Mbunge wa Mbinga Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali katika kukabiliana na changamoto za upatikanaji wa huduma za mawasiliano ya simu nchini, ilifanya tathimini katika Kata ya Kikolo inayojumuisha Vijiji vya Kikolo, Njomlole, Uzena na Luhehe na kukijumuisha Kijiji cha Kikolo katika Mradi wa Mawasiliano vijijini awamu ya tisa unaosimamiwa na Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambapo mtoa huduma ambaye ni Shirika la Mawasiliano Tanzania - TTCL anajenga mnara katika kijiji hicho na utekelezaji wa ujenzi wa mnara huo unaendelea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Kata ya Kagugu inayoundwa na Vijiji vya Kagugu, Makunguru, Mtetema, Makatani na Maganagana, Serikali kupitia mfuko wa mawasiliano kwa wote - UCSAF itafanya tathmini katika kata hii ili kupata mahitaji halisi ya huduma za mawasiliano na kuyaweka maeneo yatakayobainika kuwa na uhitaji katika mpango mkakati wa ujenzi wa minara kwa mwaka 2025/2030.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved