Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Lucy Simirya Kombani
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. LUCY D. S. KOMBANI aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuboresha miundombinu kwa wakulima wanaolima milimani Mkoa wa Morogoro ili kudhibiti upotevu wa maji?
Supplementary Question 1
MHE. LUCY S. KOMBANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na ninashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Swali langu la kwanza la nyongeza, je, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya skimu za Lupiro, Euga na Minepa ambapo Skimu hii ya Lupiro tu ikikamilika ina uwezo wa kuhudumia ekari 40,000, na hii ya Euga ikikamilika ina uwezo wa kuhudumia ekari 32,000 ambayo ni sawasawa na wakulima 82,000 watanufaika kwenye skimu hizi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili. Wilaya ya Mvomero hususan kwenye Tarafa ya Mgeta ni wakulima na wasambazaji wazuri sana wa mbogamboga pamoja na matunda, lakini wakulima hawa wamekuwa wakitumia njia za kienyeji kama kutumia mianzi ili kupitisha maji kwenye mabomba yao. Je, Serikali haioni haja ya kuwaboreshea miundombinu hii? (Makofi)
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Ninampongeza Mheshimiwa Lucy Kombani, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Morogoro kwa maswali yake mawili ya nyongeza ya msingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo moja ni kwamba kuhusu Skimu ya Lupiro na Luhuga kwamba lini tutapeleka fedha, nimwambie tu kwamba skimu hizi ziko katika mpango wa fedha wa mwaka unaokuja kuhakikisha kwamba zinaendelea kutekelezwa. Kwa hiyo, tuko katika hatua za mwisho za kuhakikisha kwamba fedha inashuka katika maeneo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye Tarafa ya Mgeta katika Jimbo la Mvomero, amesema wananchi wanatumia mianzi kama sehemu ya mabomba kupeleka maji na ameiomba Serikali kuhakikisha tunaboresha mradi huo. Nimthibitishie tu kwamba mradi huo tayari tumeshatuma wataalamu wanaofanya upembuzi yakinifu kwa ajili ya kwenda kuboresha ule mradi ili wananchi wale sasa wapatiwe miundombinu bora na ya kisasa.
Name
Hemed Sumry Haidary
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mpanda Mjini
Primary Question
MHE. LUCY D. S. KOMBANI aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuboresha miundombinu kwa wakulima wanaolima milimani Mkoa wa Morogoro ili kudhibiti upotevu wa maji?
Supplementary Question 2
MHE. HAIDARY H. SUMRY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru sana. Ninaomba kumwuliza swali Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba, je, ni lini Skimu ya Umwagiliaji ya Kakese ambayo iko kwenye Jimbo la Mpanda Mjini itaanza kujengwa? (Makofi)
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Skimu ya Kakese iliyopo katika Jimbo la Mpanda Mjini, tulikuwa tumeshamaliza upembuzi yakinifu na sasa tunakwenda katika hatua ya kuutangaza ili kupata mkandarasi na ianze kujengwa. Kwa hiyo, nimwondoe shaka tu kwamba ninaamini katika mwaka wa fedha unaokuja shughuli hiyo itaanza.
Name
Josephine Joseph Kapoma
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. LUCY D. S. KOMBANI aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuboresha miundombinu kwa wakulima wanaolima milimani Mkoa wa Morogoro ili kudhibiti upotevu wa maji?
Supplementary Question 3
MHE. JOSEPHINE J. KAPOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, wakazi wa Kata ya Boma Mlimani Luhungo wa Wilaya ya Morogoro Mjini wamekuwa na mgogoro wa muda mrefu na Serikali kwa ajili ya uharibifu wa mazingira. Je, Serikali ina mpango gani wa kuja na mkakati wa kutoa elimu ya mbinu bora za kilimo zitakazozingatia uhifadhi wa mazingira?
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nimthibitishie tu Mheshimiwa Josephine kwamba, moja ya mkakati wa Serikali ili kuhakikisha kwamba wananchi hawaendelei kuharibu mazingira, ni pamoja na kuhakikisha tunajenga miundombinu bora na ya kisasa, kwa maana ya mabwawa na schemes ili wananchi wale tukishawapanga na kuonesha maeneo ambayo wanafaa kufanya kilimo chao, maana yake hawatakuwa na nafasi ya kwenda kuharibu mazingira katika maeneo mengine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, tutaendelea kupeleka timu kwa ajili ya kuwaelimisha wananchi umuhimu wa kutunza mazingira, kwa sababu sisi mazingira ndiyo ambayo yanatusaidia kupata vyanzo bora vya maji ambavyo sasa miradi yetu ndiyo maeneo ambayo tumekuwa tukitekeleza.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved