Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza: - Je, tangu kurejeshwa kwa Export Levy kwenda Bodi ya Korosho Tanzania ni kiasi gani kimekusanywa hadi sasa na kimetumikaje?

Supplementary Question 1

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Spika, ninaomba niseme kwamba majibu yaliyojibiwa yamekuwa too general, na hizi fedha ni za wakulima, bila shaka wangetamani kufahamu kinagaubaga jinsi fedha zao zinavyotumika baada ya kukatwa.

Mheshimiwa Spika, sasa kuna majibu ya kusema kwamba wamepewa wazabuni, wamelipiwa wazabuni, lakini wazabuni hao ni wapi? Halikadhalika, zimelipwa kwa ajili ya maendeleo. Je, miradi hii ya maendeleo ni ipi, kwa sababu swali linaonekana limeulizwa vizuri, lakini majibu yamefungwafungwa. Bado tunahitaji kufahamu, ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nimshukuru Mheshimiwa Issa Ally Mchungahela, Mbunge wa Lulindi kwa maswali yake ya msingi. Sisi kama Wizara kupitia Bodi ya Korosho tuko tayari kumpatia orodha ya wazabuni wote waliolipwa pamoja na miradi ya maendeleo ambayo inatekelezwa kupitia fedha hizi za Export Levy ambazo Bodi imepokea. Kwa hiyo, kwa sababu ni orodha kubwa, tutampatia.