Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Latifa Khamis Juwakali
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. LATIFA KHAMIS JUWAKALI aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kukuza Vipaji na Ujuzi wa Vijana wa Tanzania?
Supplementary Question 1
MHE. LATIFA KHAMIS JUWAKALI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi, ili niweze kuuliza maswali mawili madogo ya ngongeza. Mheshimiwa Naibu Waziri, utaungana na mimi kwamba, katika majibu yake ya msingi kuna programu mbalimbali ambazo wamezianzisha kupitia Wizara hii. Nataka kufahamu programu hizo zilizoanzishwa, kama Wizara, imechukua hatua gani ya kuwasaidia vijana, hasa wa vijijini kuzijua fursa hizo na kuweza kuzipata kwa urahisi?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili. Kuna vijana wana vipaji mbalimbali, lakini vijana hao Serikali bado haijawatambua na kuwawezesha kiujumlajumla. Nataka kujua ni upi mpango wa Serikali wa kuwasaidia vijana hao moja kwa moja, ili zinapotoka fursa hizo waweze kuzipata kwa haraka, hususan katika mikopo mbalimbali? Ahsante sana. (Makofi)
Name
Rahma Riyadh Kisuo
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA MAHUSIANO (MHE. RAHMA R. KISUO) K. n. y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MAENDELEO YA VIJANA: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge Latifa Juwakali, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali katika kuwezesha programu hizi kuwafikia vijana wa vijijini imeanzisha utaratibu wa kutoa elimu kupitia mitandao ya kijamii, vyombo vya habari, redio na magazeti. Aidha, elimu imekuwa ikitolewa kupitia makongamano na maadhimisho mbalimbali. Vilevile, baadhi ya fursa hizi zimekuwa zikibandikwa katika mbao mbalimbali za matangazo za watendaji kata na vijiji.
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Muhsin Ussi, swali la nyongeza. Mawili, endelea.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA MAHUSIANO (MHE. RAHMA R. KISUO) K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MAENDELEO YA VIJANA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika kutambua vijana wenye vipaji na kuwaunganisha katika fursa mbalimbali Serikali, kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, katika Mfuko wa Uwezeshaji wa shilingi bilioni 200 za Mama kwa Vijana, Wizara hii imepewa jumla ya shilingi bilioni 30 za kuwawezesha vijana katika sekta ya ubunifu nchini, ikiwemo wasanii, wanamuziki, watengeneza maudhui maarufu kama content creators, influencers, waandishi wa habari na wabunifu mbalimbali wa kazi za sanaa kwa kuwapatia mikopo. Hatua inayolenga kukuza uchumi na ubunifu kwa kutoa fursa zaidi za kiuchumi kwa vijana.
Name
Muhsin Haji Ussi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Malindi
Primary Question
MHE. LATIFA KHAMIS JUWAKALI aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kukuza Vipaji na Ujuzi wa Vijana wa Tanzania?
Supplementary Question 2
MHE. MUHSIN HAJI USSI: Mheshimiwa Naibu Spika, je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha wale vijana ambao wapo vijijini hawana smartphone na hawana uwezo wa ku-access mitandao ya kijamii, wanaweza kufikiwa kwa haraka kuweza kupata taarifa husika juu ya uwepo wa fursa hizi kwa vijana Tanzania? Nakushukuru sana. (Makofi)
Name
Rahma Riyadh Kisuo
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA MAHUSIANO (MHE. RAHMA R. KISUO) K. n. y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MAENDELEO YA VIJANA: Mheshimiwa Naibu Spika, hili nimelijibu pia, kwenye swali la kwanza la nyongeza la Mheshimiwa Juwakali. Kwa wale ambao hawataweza kupata access ya social media, tunaweza kutoa elimu kupitia makongamano na maadhimisho mbalimbali. Vilevile baadhi ya fursa zimekuwa zikibandikwa katika mbao mbalimbali za matangazo za watendaji kata na vijiji.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved