Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 3 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Rais: Maendeleo ya Vijana 14 2026-04-02

Name

Latifa Khamis Juwakali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LATIFA KHAMIS JUWAKALI aliuliza:-

Je, Serikali ina mkakati gani wa kukuza Vipaji na Ujuzi wa Vijana wa Tanzania?

Name

Joel Arthur Nanauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtwara Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA MAHUSIANO (MHE. RAHMA R. KISUO) K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MAENDELEO YA VIJANA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Latifa Khamis Juwakali, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imefanya mapitio ya Sera ya Elimu na Mafunzo ya 2014, Toleo la Mwaka 2023 na Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana ya Mwaka 2007, Toleo la Mwaka 2024. Aidha, Serikali inakamilisha mapitio ya Sera ya Taifa ya Ajira ya Mwaka 2008. Lengo la kufanya mapitio hayo, ni kuimarisha utekelezaji wa sera hizo kwa kuzingatia mahitaji ya sasa na ya baadaye.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile kuanzishwa kwa Programu ya Taifa ya Kukuza Ujuzi kwa lengo la kukuza ujuzi wa nguvukazi ya Taifa, ili kumudu ushindani katika soko la ajira, ambapo hadi sasa Watanzania 168,657 wamenufaika. Vilevile, kuendeleza vituo vya ubunifu na atamizi, mashindano ya sayansi na teknolojia, pamoja na programu za kuibua na kukuza vipaji katika sekta mbalimbali.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kuwasilisha.