Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 3 | Youth, Disabled, Labor and Employment | Ofisi ya Rais: Maendeleo ya Vijana | 14 | 2026-04-02 |
Name
Latifa Khamis Juwakali
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. LATIFA KHAMIS JUWAKALI aliuliza:-
Je, Serikali ina mkakati gani wa kukuza Vipaji na Ujuzi wa Vijana wa Tanzania?
Name
Joel Arthur Nanauka
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mtwara Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA MAHUSIANO (MHE. RAHMA R. KISUO) K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MAENDELEO YA VIJANA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Latifa Khamis Juwakali, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imefanya mapitio ya Sera ya Elimu na Mafunzo ya 2014, Toleo la Mwaka 2023 na Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana ya Mwaka 2007, Toleo la Mwaka 2024. Aidha, Serikali inakamilisha mapitio ya Sera ya Taifa ya Ajira ya Mwaka 2008. Lengo la kufanya mapitio hayo, ni kuimarisha utekelezaji wa sera hizo kwa kuzingatia mahitaji ya sasa na ya baadaye.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile kuanzishwa kwa Programu ya Taifa ya Kukuza Ujuzi kwa lengo la kukuza ujuzi wa nguvukazi ya Taifa, ili kumudu ushindani katika soko la ajira, ambapo hadi sasa Watanzania 168,657 wamenufaika. Vilevile, kuendeleza vituo vya ubunifu na atamizi, mashindano ya sayansi na teknolojia, pamoja na programu za kuibua na kukuza vipaji katika sekta mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kuwasilisha.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved