Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza:- Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga Mtambo wa Refinery wa kuchakata Mafuta kwa kuwa Mradi wa Bomba la Mafuta toka Uganda unatarajia kuanza?

Supplementary Question 1

MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Naibu Spika, sijafurahishwa sana na majibu ya Serikali kwa sababu shida tunapata sisi. Leo hii kila anayesimama anazungumzia athari zinazotokana na uhaba wa mafuta na bei kupanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu niliuliza, Serikali haioni haja? Angeniambia kama Serikali haioni haja, kwa sababu uwepo wa refinery Tanzania utaongeza ajira, utatupunguzia matumizi ya fedha za nje kununua mafuta, utatuhakikishia usalama wa upatikanaji wa mafuta na kadhalika. Sasa swali langu, angalau angesema watauweka mpango huu katika Mpango wa Maendeleo ya Taifa ili kuweza kuangalia uwezekano.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Je, ni kwa nini hawataki kufanya feasibility study ambayo itaweza kuainisha umuhimu wa uwepo wa refinery, ama isiwepo refinery?
Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru sana.

Name

Salome Wyckiffe Makamba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, tunaielewa concern ya Mheshimiwa Mbunge na tunamshukuru kwa mchango wake katika sekta hii ya mafuta.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la msingi lilikuwa linahusiana na ujenzi wa refinery kwa ajili ya mradi wa bomba la mafuta linalotoka Uganda kuja Tanzania. Nimwambie Mheshimiwa Mbunge, mipango kwa ajili ya kutafuta na kutafiti mafuta na ujenzi wa refinery katika Wizara yetu ipo na utafiti unaendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hivi zipo timu ambazo zinafanya utafiti katika maeneo mbalimbali nchini; na mara tutakapopata mafuta ya kutosha na gesi ya kutosha, basi Serikali ipo tayari kwa ajili ya kujenga refinery ili kuweza kuwahudumia Watanzania, kama alivyosema kwamba refinery inatoa ajira, lakini inaleta uhakika wa mafuta ndani ya nchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru sana. (Makofi)