Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 3 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 15 2026-04-02

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza:-

Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga Mtambo wa Refinery wa kuchakata Mafuta kwa kuwa Mradi wa Bomba la Mafuta toka Uganda unatarajia kuanza?

Name

Salome Wyckiffe Makamba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Msheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Tarimba Abbas Gulam, Mbunge wa Kinondoni, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa EACOP unatekelezwa na wawekezaji binafsi (private investors) kwa kushirikiana na Serikali za Uganda na Tanzania. EACOP Ltd ni kampuni inayosimamia ujenzi na baadaye uendeshaji wa miundombinu ya mradi.

Mheshimiwa Naibu Spika, wawekezaji wamepanga kujenga mtambo wa kusafisha mafuta ghafi (refinery) kwa upande wa Uganda ambao utachakata mafuta, ambayo yatatosha soko la Uganda na nchi jirani, ikiwemo Tanzania. Naomba kuwasilisha.