Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 3 | Energy and Minerals | Wizara ya Nishati | 15 | 2026-04-02 |
Name
Tarimba Gulam Abbas
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kinondoni
Primary Question
MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza:-
Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga Mtambo wa Refinery wa kuchakata Mafuta kwa kuwa Mradi wa Bomba la Mafuta toka Uganda unatarajia kuanza?
Name
Salome Wyckiffe Makamba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Msheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Tarimba Abbas Gulam, Mbunge wa Kinondoni, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa EACOP unatekelezwa na wawekezaji binafsi (private investors) kwa kushirikiana na Serikali za Uganda na Tanzania. EACOP Ltd ni kampuni inayosimamia ujenzi na baadaye uendeshaji wa miundombinu ya mradi.
Mheshimiwa Naibu Spika, wawekezaji wamepanga kujenga mtambo wa kusafisha mafuta ghafi (refinery) kwa upande wa Uganda ambao utachakata mafuta, ambayo yatatosha soko la Uganda na nchi jirani, ikiwemo Tanzania. Naomba kuwasilisha.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved