Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Hemed Sumry Haidary
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mpanda Mjini
Primary Question
MHE. HAPPINESS D. NGWANDO K.n.y. MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza: - Je, lini ujenzi wa Soko la Mfaranyaki katika Manispaa ya Songea utaanza kwa kuwa hali iliyopo ni hatarishi kwa usalama wa watumiaji?
Supplementary Question 1
MHE. HAIDARY H. SUMRY: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Manispaa ya Mpanda ni miongoni mwa Manispaa ambazo zilipata mradi wa TACTIC na katika mradi huo tulikuwa na miradi miwili; mradi wa barabara, na mradi wa soko la kisasa pale Kazima. Mradi wa barabara tayari tulishaanza, na mradi wa soko bado haujaanza.
Mheshimiwa Spika, nilitaka kuiuliza Serikali, ni lini mradi wa soko la kisasa la Kazima utaanza kujengwa?
Name
Kwagilwa Reuben Nhamanilo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Handeni Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO): Mheshimiwa Spika, kama alivyotangulia kuuliza, Serikali imefanya kazi kubwa sana kupitia mradi huu wa TACTIC. Kwenye eneo analotoka Mheshimiwa Mbunge, zimejengwa barabara za lami karibu kilomita 13 kwa zaidi ya shilingi bilioni 23.
Mheshimiwa Spika, awamu ya pili itakayofuata itakuwa ni ujenzi wa soko, na tumefanya hivyo kwenye TACTIC awamu ya kwanza, maeneo ambayo tulianza na barabara awamu ya pili tulianza na ujenzi wa soko. Maeneo ambayo tulianza na ujenzi wa masoko awamu ya pili tulianza na ujenzi wa barabara.
Mheshimiwa Spika, ninaomba kuwasilisha.
Name
Zainab Rashid Kawawa
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. HAPPINESS D. NGWANDO K.n.y. MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza: - Je, lini ujenzi wa Soko la Mfaranyaki katika Manispaa ya Songea utaanza kwa kuwa hali iliyopo ni hatarishi kwa usalama wa watumiaji?
Supplementary Question 2
MHE. ZAINAB R. KAWAWA: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru. Katika Mkoa wa Lindi, Halmashauri za Wilaya za Liwale, Nachingwea, Ruangwa, Mtama pamoja na Kilwa, hazina masoko ya kisasa. Je, ni nini mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba Halmashauri hizi zinajengwa masoko ya kisasa?
Name
Kwagilwa Reuben Nhamanilo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Handeni Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO): Mheshimiwa Spika, utaratibu wa masoko ya kimkakati huwa yanaanza na andiko kutoka kwenye Halmashauri husika. Andiko hilo huwasilishwa TAMISEMI, nasi kwenye Wizara yetu hufanya mapitio na baadaye kulipeleka kwenye Wizara ya Mipango ambao wakiridhia hulifikisha Wizara ya Fedha kwa ajili ya kupatiwa fedha na kuanza kutekelezwa.
Mheshimiwa Spika, hivyo, kwa uhitaji alioutaja Mheshimiwa Mbunge wa Mkoa wa Lindi, ninawaelekeza Wakurugenzi wa maeneo yote yaliyotajwa kuwa na ushirikiano na wawakilishi wa wananchi ili kufuata hatua hizo na hatimaye Serikali iweze kuwahudumia wananchi wa maeneo hayo.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved