Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 2 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) | 3 | 2026-04-01 |
Name
Jacqueline Ngonyani Msongozi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. HAPPINESS D. NGWANDO K.n.y. MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza: -
Je, lini ujenzi wa Soko la Mfaranyaki katika Manispaa ya Songea utaanza kwa kuwa hali iliyopo ni hatarishi kwa usalama wa watumiaji?
Name
Kwagilwa Reuben Nhamanilo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Handeni Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO) alijibu: -
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Jacqueline Ngonyani, Mbunge wa Mkoa wa Ruvuma, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Spika, Soko la Mfaranyaki ni soko la muda lililotengwa pamoja na maeneo ya Mji Mwema na Bombambili, kwa ajili ya kuhifadhi wafanyabiashara waliopisha ujenzi wa Masoko ya Manzese A na B katika Manispaa ya Songea.
Mheshimiwa Spika, ujenzi wa masoko ya kudumu ya Manzese A na B unaendelea kwa gharama ya shilingi bilioni 23.5 na unatarajiwa kukamilika ifikapo Disemba, 2026. Masoko hayo yakikamilika yatatumika kwa wafanyabiashara walioondolewa kupisha ujenzi na wafanyabiashara wengine.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Mfaranyaki ni eneo la muda na halina miundombinu stahiki, wafanyabiashara wanakabiliwa na changamoto za kutokuwepo kwa jengo la wafanyabiashara, hivyo kusababisha kutiririka kwa maji, usalama mdogo, na kushindwa kudumisha ubora wa bidhaa zinazouzwa katika soko hilo.
Mheshimiwa Spika, katika kukabiliana na changamoto hiyo, Serikali kupitia Halmashauri ya Manispaa ya Songea imetenga shilingi milioni 80 katika bajeti ya mwaka 2026/2027 kwa ajili ya ujenzi wa paa katika soko la Mfaranyaki wakati tukisubiri kukamilika kwa ujenzi wa masoko ya kudumu ya Manzese A na B.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved