Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Neema Gerald Mwandabila
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza: - Je, upi mpango wa Serikali katika kuhakikisha hospitali zote za Wilaya, Vituo vya Afya na Zahanati zinakuwa na uzio?
Supplementary Question 1
MHE. NEEMA G. MWANDABILA: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa, ujenzi wa uzio katika vituo vya afya na hospitali zetu huko Halmashauri haujawa kipaumbele, ni ipi kauli ya Serikali kuzielekeza Halmashauri zijenge uzio kwenye vituo vya afya, zahanati pamoja na hizo hospitali za Wilaya?
Mheshimiwa Spika, pia, ninatamani kufahamu, ni upi mpango wa Serikali kupeleka zile fedha ambazo ilikuwa imeahidi kumalizia katika Kituo cha Kamsamba Jimbo la Momba? Ahsante.
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Spika, kama nilivyoeleza kwenye majibu yangu ya msingi, kipaumbele cha Serikali hasa katika hivi vituo vyetu vya afya na zahanati zetu ni kuhakikisha angalau zile huduma za maternity complex, kuokoa maisha ya mama na mtoto. Pia, hatujaacha nyuma kujenga uzio katika maeneo yote ya hospitali.
Mheshimiwa Spika, ninampongeza Mheshimiwa Neema kwa kuendelea kuwasemea wananchi hawa, nasi tutaendelea kupeleka bajeti kwa ajili ya kujenga uzio.
Mheshimiwa Spika, jambo la pili aliloelezea kuhusu hiki kituo cha afya, tayari tumeshazungumza kwenye vikao vyetu vya halmashauri, na tulikutana na Wakurugenzi ili kuhakikisha zile fedha ambazo Serikali imezielekeza, ni kweli ziende zikafanye kazi ya kumalizia ujenzi wa kituo cha afya.
Name
Azza Hilal Hamad
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza: - Je, upi mpango wa Serikali katika kuhakikisha hospitali zote za Wilaya, Vituo vya Afya na Zahanati zinakuwa na uzio?
Supplementary Question 2
MHE. AZZA H. HAMAD: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru kwa kunipa nafasi hii ya kuweza kuuliza swali la nyongeza. Kituo cha Afya cha Tinde kimezungukwa na barabara kuu tatu; barabara iendayo Dar es Salaam, Kahama na Mwanza. Kituo hiki hakina uzio. Je, ni nini mpango mkakati wa Serikali kuhakikisha Kituo cha Afya cha Tinde kinajengewa uzio?
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Spika, kwanza ninampongeza Mheshimiwa Azza kwa kuwapambania wananchi wa Jimbo la Itwangi. Kituo cha Afya cha Tinde ni njia yangu ya kuelekea Jimboni Busanda. Huwa mara zote ninapita pale na tunajionea sote kwa sababu kile kituo kiko njiani.
Mheshimiwa Spika, nilifanya ziara katika kituo hiki cha afya, hakika kinahitaji uzio kwa maana ya kwamba kipo karibu sana na barabara. Pia tunawaomba wenzetu wa TANROADS waweze kuzungumza na wale wafanyabiashara waliopo katika kingo ile ya barabara ili kukipa nafasi kituo na kuendelea kutenga bajeti.
Mheshimiwa Spika, nimeshafanya mawasiliano na Mkurugenzi ili kuweza kutenga bajeti na kufanya tathmini ya uzio huu na hitaji la kibajeti ili tuone namna gani ya kuweza kuanza kujenga uzio.
Name
Amosy William Maganga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Sikonge
Primary Question
MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza: - Je, upi mpango wa Serikali katika kuhakikisha hospitali zote za Wilaya, Vituo vya Afya na Zahanati zinakuwa na uzio?
Supplementary Question 3
MHE. ENG. AMOSY W. MAGANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Je, ni lini kituo chetu cha afya kilichopo Kata ya Kipili, Jimbo la Sikonge, kitajengewa jengo la wagonjwa wa nje (OPD)?
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Spika, Serikali tumejielekeza katika mwaka huu wa fedha angalau kukamilisha majengo ya OPD katika vituo hivi vya afya na yaanze kutoa huduma. Ninamhakikishia Mheshimiwa Mbunge, katika mwaka huu wa fedha tutakamilisha jengo hilo la OPD na lianze kutoa huduma.
Mheshimiwa Spika, ninaomba kuwasilisha.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved