Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 2 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) | 2 | 2026-04-01 |
Name
Neema Gerald Mwandabila
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza: -
Je, upi mpango wa Serikali katika kuhakikisha hospitali zote za Wilaya, Vituo vya Afya na Zahanati zinakuwa na uzio?
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF) alijibu: -
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Neema Gerald Mwandabila, Mbunge Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, uzio ni hitaji muhimu kwenye vituo vyetu vya kutolea huduma za afya nchini kwa ajili ya usalama wa watoa huduma wetu, wagonjwa, jamii inayozunguka vituo vya kutolea huduma za afya, mali pamoja na kuzuia uvamizi wa ardhi ya kituo. Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI tayari imetoa maelekezo kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa kuhakikisha maeneo yote ya taasisi za umma, hususan vituo vya huduma za afya na shule yanapimwa na kutengenezewa hatimiliki.
Mheshimiwa Spika, pamoja na umuhimu wa uzio kwenye vituo vya kutolea huduma za afya, kwa sasa Serikali imejielekeza katika kukamilisha miundombinu muhimu ya kutolea huduma za afya, ikiwemo jengo pacha la huduma za uzazi/upasuaji, jengo la kufulia, wodi na jengo la kuhifadhia maiti. Aidha, Serikali kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri itaendelea kutenga fedha kwa awamu kwa ajili ya ujenzi wa uzio kwenye vituo vya kutolea huduma za afya kote nchini.
Mheshimiwa Spika, ninaomba kuwasilisha.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved