Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Kangi Alphaxard Lugola
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mwibara
Primary Question
MHE. KANGI A. LUGOLA aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha maboma 49 ya madarasa ya shule za msingi na maboma matatu ya zahanati za vijiji vitatu vya Jimbo la Mwibara?
Supplementary Question 1
MHE. KANGI A. LUGOLA: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa majibu niliyojibiwa ni tofauti na swali nililouliza, ninauliza swali moja tu la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kuja Mwibara ili aone nilichouliza cha maboma ya zahanati ya Kigaga, Nambugi na Sikiro, na maboma niliyouliza ya shule ya msingi Mwibara, Sunsi, Gwanza, Busambu, Mwiruruma, Mgara ‘A’ na ‘B’, Sikiro, Majoro, Igundu, Buramba, Berendabufwe na Marama, Kasaunga, Masaunga na Magunga, Kenkombe pamoja na Nampangala ili baadaye afanyie kazi aone utofauti wa alichonijibu na kile nilichouliza? Je, yuko tayari?
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Spika, kwanza ninampongeza sana Mheshimiwa Kangi Lugola kwa kazi kubwa anayoifanya kuwasemea Wananchi wa Jimbo la Mwibara.
Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, tumekuwa tukifanya ziara tukiongozwa na Mheshimiwa Waziri Mkuu. Mimi na Mheshimiwa Mbunge tutafika Jimboni Mwibara na kujionea maboma hayo. Ninamhakikishia Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Jimbo la Mwibara kwamba Serikali imejielekeza kukamilisha maboma haya na tutaendelea kutenga fedha.
Name
Dr. Christina Christopher Mnzava
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. KANGI A. LUGOLA aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha maboma 49 ya madarasa ya shule za msingi na maboma matatu ya zahanati za vijiji vitatu vya Jimbo la Mwibara?
Supplementary Question 2
MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa, tatizo hili la maboma hata katika Jimbo la Itwangi na Solwa ni changamoto kubwa sana. Ni upi mpango mkakati endelevu wa kuhakikisha kwamba yale maboma yaliyoanza kujengwa na wananchi yanakamilika?
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Spika, kwanza Serikali inatambua nguvu za wananchi na tunaendelea na utekelezaji wa kuhakikisha maboma haya yote yanakamilika. Mkakati endelevu na wa kudumu, kwanza tumesitisha uanzishwaji wa maboma mengine mapya na tunahakikisha tunakamilisha maboma yote ambayo tumeanzisha katika Majimbo yetu.
Name
Ester Amos Bulaya
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. KANGI A. LUGOLA aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha maboma 49 ya madarasa ya shule za msingi na maboma matatu ya zahanati za vijiji vitatu vya Jimbo la Mwibara?
Supplementary Question 3
MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru kwa nafasi nami niulize swali dogo la nyongeza. Maeneo ambayo pia yana changamoto ya kuwa na maboma kwenye sekta ya elimu pamoja na afya ni pamoja na Jimbo la Bunda Mjini. Ni lini sasa watamalizia ili wananchi wapate huduma ya afya na elimu?
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Spika, hata kupitia katika randama zetu za mikoa, tumekuwa tukielekeza kwamba tutenge bajeti hasa katika Halmashauri zetu ili kukamilisha maboma haya. Pia, upo mpango mkakati wa Serikali kupitia fedha za ruzuku ili kuhakikisha tunakamilisha maboma haya nchi nzima.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved