Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza: - Je, lini Serikali itafanya ukarabati au kuliongeza Gereza la Keko?

Supplementary Question 1

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nishukuru sana kwa jinsi ambavyo fedha hizi zimeweza kushushwa. Sina swali la nyongeza, lakini napenda kumshukuru sana Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, na Serikali yake ya Chama cha Mapinduzi kwa jinsi ambavyo hakika tumeweza kuomba na fedha hizi na zimeshuka. Muhimu ni kwamba, tunaomba sasa Jeshi la Magereza lifanye kazi kwa udhibiti, ili gereza lile lipate kuwa na usafi na usalama.

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sana Mheshimiwa Dorothy Kilave, Mbunge wa Temeke, kwa ufuatiliaji wake. Pia, namshukuru sana kwa kutambua kazi kubwa inayofanywa na Dkt. Samia Suluhu Hassan katika ukarabati wa magereza mbalimbali hapa nchini. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza: - Je, lini Serikali itafanya ukarabati au kuliongeza Gereza la Keko?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Gereza la Wilaya ya Mbulu limejengwa toka enzi za koloni. Kwa Bahati nzuri na Serikali imekuwa na mipango mizuri ya kukarabati magereza haya kongwe nchini. Mpango ukoje kwa magereza yote nchini, likiwemo Gereza la Wilaya ya Mbulu, katika ukarabati na ujenzi wa makazi ya Askari na jengo la magereza? (Makofi)

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, mkakati wa Serikali ni kuhakikisha kila mwaka wa fedha tunatenga fedha kwa ajili ya ukarabati wa magereza mbalimbali. Kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025 tulitenga shilingi bilioni 6.272, kwa ajili ya ukarabati wa magereza haya. Tumeanza na Gereza la Keko, Ukonga, Segerea pamoja na Gereza la Lilungu liliopo Mkoa wa Mtwara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge pia, kama nilivyosema, tunatenga fedha kila mwaka. La Mbulu pia, tutalichukua tuliingize kwenye mpango, tayari kwa ajili ya kutengewa fedha ya ukarabati. Ahsante sana.

Name

Maryam Omar Said

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Pandani

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza: - Je, lini Serikali itafanya ukarabati au kuliongeza Gereza la Keko?

Supplementary Question 3

MHE. MARYAM OMAR SAID: Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na hali isiyoridhisha ya makazi ya Askari wa Finya, Basara pamoja na Wetelaini, ni lini Serikali ifanya ukarabati mkubwa wa makazi hayo?

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa ikitenga fedha kila mwaka na kufanya ukarabati wa makazi ya Askari wetu. Namhakikishia Mheshimiwa Mbunge, pia maeneo aliyoyataja ya Finya pamoja na Wete wataalamu wetu wataenda kufanya tathmini, ili kuona kiasi kinachotakiwa na kutenga fedha kwa ajili ya ukarabati. Askari wetu wakae katika mazingira salama kwa ajili ya kulinda raia na mali zao. Ahsante sana.

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza: - Je, lini Serikali itafanya ukarabati au kuliongeza Gereza la Keko?

Supplementary Question 4

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa, uwepo wa magereza katika maeneo mbalimbali umesaidia sana kuongeza nguvukazi, hasa katika masuala ya usafi na mambo mengine, maeneo ya miji. Je, ni lini Gereza la Wilaya ya Nyasa, ambalo tayari Wizara imeshalipa fidia, litaanza kujengwa ili pia, Nyasa inufaike na uwepo wa magereza?

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Mhandisi Stella Manyanya kwa ufuatiliaji wake wa Gereza la Nyasa. Namhakikishia Mheshimiwa Mbunge, tayari kama ambavyo Serikali imelipa fidia, ndiyo hiyo hatua ya kwanza. Kulipia fidia ni kuwaondoa wananchi katika eneo hilo na sasa hatua inayofuata ni kutenga fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Gereza la Nyasa. Ahsante sana.