Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 53 | Home Affairs | Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi | 681 | 2025-06-25 |
Name
Dorothy George Kilave
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Temeke
Primary Question
MHE. DOROTHY G. KILAVE aliuliza: -
Je, lini Serikali itafanya ukarabati au kuliongeza Gereza la Keko?
Name
Daniel Baran Sillo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Babati Vijijini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Gereza la Mahabusu Keko ni miongoni mwa Magereza yaliyojengwa katika kipindi cha ukoloni, mwaka 1957. Serikali kupitia Jeshi la Magereza imepokea fedha kiasi cha shilingi 988,125,000.00 kilichotengwa katika mwaka wa fedha 2024/2025, kwa ajili ya ukarabati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa Jeshi la Magereza linaendelea na hatua mbalimbali za manunuzi kwa ajili ya kuanza kazi ya ukarabati wa gereza hilo, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved