Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Gereza la Wilaya ya Kishapu?

Supplementary Question 1

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Mwaka wa fedha 2024/2025, Serikali iliweka katika mpango wa bajeti kutekeleza ujenzi wa Magereza hii ya Wilaya ya Kishapu lakini kwa bahati mbaya mpaka hatua hii ya mwisho utekelezaji wake haujatekelezwa. Je, Serikali iko tayari kuwahakikishia wananchi wa Kishapu kwamba Magereza hii itaenda kujengwa katika mwaka wa fedha unaokuja (2025/2026)? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kuna changamoto kubwa ya usafiri na hasa kwa wale mahabusu ambao wanakuwa na mashauri katika Mahakama iliyopo katika Wilaya ya Kishapu na inawabidi wasafirishwe kwenda Manispaa ya Shinyanga kuliko na Magereza ya Mkoa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa Serikali iko tayari kuhakikisha kwamba inawapatia Mahakama ya Wilaya ya Kishapu na magereza kuhakikisha kwamba wanapata usafiri ambao utasaidia mahabusu hukudhuria mashauri kwa wakati bila usumbufu wa aina yoyote? (Makofi)

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa ufuatiliaji wake katika ujenzi wa gereza katika eneo la Kishapu. Ni kweli, kwa mwaka wa fedha 2024/2025, Gereza la Kishapu lilikuwa limewekwa kwenye mpango, lakini halikutengewa bajeti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge pamoja na wananchi wa Kishapu kwamba kwa mwaka wa fedha 2026/2027 ndiyo tunatenga bajeti kwa ajili ya ujenzi wa magereza hapo Kishapu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu gari, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari tumeshaagiza magari 11, kwa takribani shilingi bilioni 2.5. Basi Wizara ya Kishapu pia tutaiweka kwenye mpango ili wapate gari kwa ajili ya kusafirisha mahabusu kwenda kusikiliza mashauri yao katika Halmashauri ya Shinyanga, ahsante. (Makofi)

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Gereza la Wilaya ya Kishapu?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna magereza ambayo yapo kwa ajili ya wafungwa kwa maana ya uzalishaji wa kilimo na mifugo takribani saba nchini yaliyojengwa enzi ya miaka ya 1970 ni ya matope, lakini sasa hivi yana wafungwa wachache, Askari Magereza wengi, hivyo hayana tija katika uzalishaji. Serikali haioni kwamba kuna umuhimu sasa wa kupunguza magereza haya yabaki walau mawili ili yaweze kuzalisha kwa tija? (Makofi)

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Esther ametoa ushauri na sisi kama Serikali tunaupokea ushauri huo kwenda kuufanyia kazi tuone namna ya kuboresha eneo hilo, ahsante. (Makofi)

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Gereza la Wilaya ya Kishapu?

Supplementary Question 3

MHE. STELLA S. FIYAO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashukuru sana. Magereza nyingi nchini zina hali mbaya sana na ni chakavu. Ni upi mkakati wa Serikali kuhakikisha mnakarabati Magereza haya ili yawe katika hali nzuri au kujenga Magereza mpya nzuri na za kisasa ambazo zinaendana na wakati?

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, mkakati wa Serikali ni kuzikarabati Magereza zote, ndiyo maana hata mwaka wa fedha huu wa 2025/2026 tumetenga shilingi bilioni 6.27 kwa ajili ya kufanyia ukarabati Gereza la Keko, Segerea, pamoja na Lilungu lililoko Mkoa wa Mtwara, ahsante.

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Gereza la Wilaya ya Kishapu?

Supplementary Question 4

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa nafasi. Gereza la Mji wa Babati ni gereza linalotumika na Mkoa mzima wa Manyara; na wafungwa na mahabusu wamekuwa ni wengi, nafasi hazitoshi kabisa. Je, nini mkakati wa Serikali kujenga Gereza la Mji wa Babati ambalo ni la Mkoa? (Makofi)

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Gereza la Babati ni dogo na kama alivyosema lina msongamano mkubwa, lakini tutaliweka kwenye mpango wa Gereza la Mkoa wa Manyara ili tuhakikishe tunajenga gereza kubwa linalotosheleza mahabusu pamoja na wafungwa katika eneo hilo, ahsante. (Makofi)

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tanganyika

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Gereza la Wilaya ya Kishapu?

Supplementary Question 5

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Gereza la Kilimo la Kalilankulukulu ni gereza la muda mrefu, lina uchakavu wa hali ya juu na halina nyumba za watumishi. Je, ni lini Serikali itaenda kupeleka fedha za ukarabati wa gereza na kujenga nyumba za watumishi? (Makofi)

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema, Serikali ina mpango wa kukarabati hayo Magereza, lakini hatuwezi kukarabati kwa mwaka mmoja. Kwa hiyo, kila mwaka tunatenga bajeti kwa mwaka. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, pia gereza lake ambalo amelitaja, tutaliweka kwenye mpango ili kutengewa fedha kwa ajili ya ukarabati wa uhakika, ahsante. (Makofi)

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Gereza la Wilaya ya Kishapu?

Supplementary Question 6

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Lini Mheshimiwa Naibu Waziri atakuwa tayari kutembelea Gereza letu zuri la Kiberege kujionea miradi yetu mizuri na kuunga mkono miradi ya gereza? (Makofi)

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nitakaa na Mheshimiwa Mbunge ili tupange namna ya kwenda kuona kazi kubwa inayofanyika katika gereza hilo, ahsante sana. (Makofi)