Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 37 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 479 2025-06-02

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: -

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Gereza la Wilaya ya Kishapu?

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Kishapu iliyopo Mkoa wa Shinyanga ni miongoni mwa wilaya 50 nchini ambazo hazina Magereza. Aidha, mchakato wa maandalizi ya ujenzi wa Gereza la Wilaya Kishapu umekamilika sambamba na upatikanaji wa eneo la ekari 200 na zoezi la kuwalipa fidia wananchi wanaopisha eneo la ujenzi wa gereza limekamilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ujenzi wa Gereza hilo utaanza kutekelezwa katika mwaka wa fedha 2026/2027 kupitia mpango mahsusi wa ujenzi wa magereza mapya kwenye wilaya zisizokuwa na magereza nchini, ahsante. (Makofi)