Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hassan Seleman Mtenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga mnara katika Eneo la Mbawala Chini, Kata ya Naliendele, Manispaa ya Mtwara Mikindani? (Makofi)

Supplementary Question 1

MHE. HASSAN S. MTENGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nakushukuru kwa nafasi. Pia naishukuru Serikali kwa majibu mazuri na ninamshukuru Naibu Waziri kwa kweli kazi anayoifanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kweli Serikali imejenga minara maeneo tajwa, lakini eneo la Naliendele ya Chini, tukizungumza maeneo ya Naulongo, na kuelekea mpaka kwenye hospitali ya kanda pale hakuna mawasiliano. Je, ni lini Serikali itakuja kutujengea minara hiyo ili hospitali ya kanda na maeneo mengine niliyoyazungumza tupate mawasiliano? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nipokee shukrani za Mheshimiwa Mbunge, na pia nikushukuru kwa kunipongeza mimi binafsi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika maeneo haya aliyoyataja Mheshimiwa Mbunge, nikuhakikishie mwaka ujao wa fedha (2025/2026) tutahakikisha Maeneo ya Naliendele ya Chini yanaweza kujengewa minara, mawasiliano yawe ya uhakika. Vilevile, kwenye hospitali ya kanda, wito wetu ni kuhakikisha maeneo yote yanayotoa huduma za umma kama hospitali na shule yanapata mawasiliano ya uhakika. (Makofi)

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga mnara katika Eneo la Mbawala Chini, Kata ya Naliendele, Manispaa ya Mtwara Mikindani? (Makofi)

Supplementary Question 2

MHE. ATHUMAN A. MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Kwanza, nitoe pongezi kwa Serikali kutujengea mnara mzuri sana pale Mwakashindye. Nina swali la nyongeza. Lini Serikali itajenga mnara katika Kijiji cha Mbeya, Kata ya Igulungu?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Maige kwa ufuatiliaji, na juzi tu tulikuwa pamoja jimboni kwake kwenye ziara ya kuhakikisha mawasiliano yanapatikana maeneo yote. Kijiji cha Mbeya kipo kwenye utaratibu, mwaka ujao wa fedha (2025/2026) na chenyewe tutakifikia kuhakikisha mawasiliano yanakaa vizuri. (Makofi)

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga mnara katika Eneo la Mbawala Chini, Kata ya Naliendele, Manispaa ya Mtwara Mikindani? (Makofi)

Supplementary Question 3

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwezesha hii mitandao ya simu iwe inaingiliana, badala ya sasa hivi mtu kwa wilaya kubwa kama ya Hanang ili uwe na uhakika wa kupata mawasiliano kila sehemu lazima uwe na simu zaidi ya nne? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, tayari mkakati unafanya kazi. Tumeshawaelekeza watoa huduma kama mwenzake ameshajenga mnara pale, basi waweze kutumia ule mnara kwa umoja wao. Vilevile tayari tunao mkakati wa kuona kwamba unatumia line moja kwa watoa huduma wote, pia michakato inaendelea. Lengo ni kuhakikisha mtu anatumia simu moja kumpunguzia mizigo. (Makofi)

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga mnara katika Eneo la Mbawala Chini, Kata ya Naliendele, Manispaa ya Mtwara Mikindani? (Makofi)

Supplementary Question 4

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimwulize Mheshimiwa Waziri kwamba, ni lini mtarekebisha mawasiliano kutoka Njombe mpaka Songea? Maana yake pale katikati tukifika tu Njombe, ndiyo hatuwezi kuwasiliana kabisa na ndugu. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Dkt. Thea Ntara kwa ufuatiliaji wa mawasiliano ya uhakika eneo la Njombe – Songea, naomba niwe nimepokea. Wataalam watakwenda kulifanyika tathmini na kuhakikisha linafanyiwa kazi. (Makofi)

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga mnara katika Eneo la Mbawala Chini, Kata ya Naliendele, Manispaa ya Mtwara Mikindani? (Makofi)

Supplementary Question 5

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nilitaka kujua kwamba ni lini Serikali itatujengea mnara kwenye Kijiji cha Masileye kwenye Kata ya Pagwi? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nimpongeze Mheshimiwa Omari Kigua; lengo la Serikali ni kuhakikisha vijiji vyote tunavifikia na kupata mawasiliano ya uhakika. Kwa hiyo, Kijiji hiki alichokitaja Mheshimiwa Mbunge, Masileye na chenyewe tutahakikisha mwaka ujao wa fedha (2025/2026) kinakuja kufanyiwa tathmini na kuhakikisha mawasiliano ya uhakika yanawafikia. (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga mnara katika Eneo la Mbawala Chini, Kata ya Naliendele, Manispaa ya Mtwara Mikindani? (Makofi)

Supplementary Question 6

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Je, ni lini Serikali itahakikisha kwamba mtandao wa mawasiliano ya simu yanapatikana along the way SGR yote kuanzia Dodoma mpaka Dar es Salaam? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Kandege kwa ufuatiliaji wa mawasiliano ya uhakika. Katika barabara nzima ya SGR tayari wataalam wamefanya tathmini, na kazi inaendelea kuhakikisha barabara nzima toka tunavyotokea Dodoma mpaka Dar es Salaam watu waweze kupatikana bila kukatika mahali popote. (Makofi)