Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 37 | Information, Communication and Information Technology | Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari | 478 | 2025-06-02 |
Name
Hassan Seleman Mtenga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mtwara Mjini
Primary Question
MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: -
Je, lini Serikali itajenga mnara katika Eneo la Mbawala Chini, Kata ya Naliendele, Manispaa ya Mtwara Mikindani? (Makofi)
Name
Maryprisca Winfred Mahundi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Kata ya Naliendele ipo Minara ya Mawasiliano ya simu iliyojengwa na watoa huduma ambao ni Kampuni ya Airtel, Vodacom na Honora. Minara hii inatoa huduma kwa wananchi kama ilivyokusudiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Mheshimiwa Mbunge ameuliza swali kuhusu kujengwa kwa mnara katika kata tajwa, inaashiria kuwa bado kuna changamoto ya upatikanaji wa mawasiliano ya simu. Wizara kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) itafanya tathmini kwenye kata tajwa ili kubaini mahitaji halisi ya mawasiliano ya simu, na endapo ikibainika kuwepo kwa tatizo la mawasiliano katika kata husika, itaingizwa katika zabuni ya miradi itakayotekelezwa katika mwaka wa fedha 2025/2026. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved