Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA K.n.y. MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza: - Je, lini Visima vilivyochimbwa katika Kata za Mlingula, Mkwapa na Namatutwe – Masasi vitawekwa pampu?

Supplementary Question 1

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Spika, pamoja na maswali mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini yeye mwenyewe aliahidi maji katika Kata ya Lipumburu, Kijiji cha Lipumburu wakati tulipokuwa tumefanya naye mkutano kwenye Kijiji cha Lupaso, je, anatekeleza lini ahadi hii ya uchimbaji wa kisima katika kata hii?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, kati ya mikoa ambayo Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amewekeza fedha nyingi sana, ni katika huu Mkoa wa Mtwara ikiwemo mradi wa Makonde, mradi wa kutoka Ruvuma kwenda Mangaka Nanyumbu, mradi wa kuboresha miundombinu; na pia eneo lile ambalo Mheshimiwa Mbunge ametaja. Ni kweli kabisa nilifika mimi mwenyewe Lupaso na ni ahadi ya Serikali kwamba ni lazima kisima kichimbwe kulingana na upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa Serikali inaendelea kuhakikisha kwamba fedha zipatikane ili tukatekeleze ahadi hiyo ya Serikali, ahsante sana.