Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 45 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 582 | 2025-06-12 |
Name
Agnes Elias Hokororo
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA K.n.y. MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza: -
Je, lini Visima vilivyochimbwa katika Kata za Mlingula, Mkwapa na Namatutwe – Masasi vitawekwa pampu?
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -
Mheshimiwa Spika, ninakushukuru sana. Nia ya Serikali ni kuhakikisha huduma ya majisafi, salama na yenye kutosheleza inapatikana kwa wananchi wote nchini ikiwemo wananchi wa Kata za Mlingula na Namatutwe zilizopo Wilayani Masasi Mkoa wa Mtwara. Katika kutimiza azma hiyo Serikali imekamilisha zoezi la ufungaji wa pampu kwenye visima vyote tisa vilivyochimbwa kwenye kata hizo na vimeanza kutoa huduma iliyokusudiwa kwa wananchi.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved