Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Rashid Abdallah Shangazi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mlalo
Primary Question
MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza: - Je, kipi chanzo mahsusi cha fedha za kugharamia huduma ya afya kwa mama mjamzito na mtoto chini ya miaka mitano?
Supplementary Question 1
MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu ya Serikali, lakini nina swali la nyongeza Kwa kuwa Serikali kupitia Sera ya Afya ina utaratibu wa kuanzisha mifuko mahsusi kwa ajili ya kusaidia hasa katika haya maeneo ambayo yana uhitaji mkubwa, kwa mfano hili la mama mjamzito pamoja na watoto chini ya miaka mitano, Serikali haioni sasa kuna umuhimu ikaleta utaratibu wa kutengeneza mfuko mahsusi ambao utabeba jukumu hili? (Makofi)
Name
Dr. Godwin Oloyce Mollel
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Siha
Answer
NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Shangazi kwa swali lake hili la msingi hasa kwenye hili eneo ambalo kidogo utekelezaji wake unahitaji umakini wa hali ya juu. Wazo lake tunalichukua na kwenda kulifanyia kazi kama ambavyo amelipendekeza, tuone ni namna gani tunaweza tukashirikiana na wadau mbalimbali na kuunda huo mfumo.
Name
Pauline Philipo Gekul
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Babati Mjini
Primary Question
MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza: - Je, kipi chanzo mahsusi cha fedha za kugharamia huduma ya afya kwa mama mjamzito na mtoto chini ya miaka mitano?
Supplementary Question 2
MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi. Mheshimiwa Naibu Waziri, ni vifaatiba vipi au dawa zipi mama mjamzito anayejifungua kwa operation anapaswa kulipia, kwa maana sasa wanachajiwa? Ni zipi hasa ambazo wanapaswa kulipia? (Makofi)
Name
Dr. Godwin Oloyce Mollel
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Siha
Answer
NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, kulingana na Sera ya Afya hakuna mama mjamzito anayetakiwa kupata huduma zote bure, lakini kama ambavyo nimekwishasema hapa Bungeni kwa sababu ya changamoto mbalimbali, imewezekana kuwalipia bure 65% ya akina mama, lakini 35% wamekuwa wakipata changamoto mbalimbali kutokana na masuala ya kibajeti, lakini pia na uzembe wa utendaji katika maeneo husika.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nadhani siyo kwamba ni la kusema specific hiki na hiki kinatakiwa kilipiwe, na hiki hakitakiwi kulipiwa. Mama mjamzito kulingana na sera, anatakiwa kupata huduma. Tukishirikiana na hospitali zetu pamoja na Serikali za maeneo husika kwa maana ya wilaya husika au mkoa husika, tunaweza tukapunguza hili tatizo kwa pamoja.
Name
Salma Rashid Kikwete
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Mchinga
Primary Question
MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza: - Je, kipi chanzo mahsusi cha fedha za kugharamia huduma ya afya kwa mama mjamzito na mtoto chini ya miaka mitano?
Supplementary Question 3
MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Huduma ya afya kwa mama mjamzito na watoto ni jambo muhimu na la msingi katika kunusuru changamoto zinazojitokeza kwa watoto hawa na mama yao. Sasa, je, ni lini Serikali itatupatia fedha ili kuweza kujenga Kituo cha Afya kule Nangaru, ili mama mjamzito na watoto hawa waweze kupata huduma hizo? (Makofi)
Name
Dr. Godwin Oloyce Mollel
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Siha
Answer
NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge mama yetu Salma Kikwete, moja kwa kazi kubwa sana wakati akiwa First Lady aliyoifanya kwenye eneo la mtoto wa kike, amefanya kazi kubwa sana. Pia kwa kazi kubwa anayoendelea kuifanya kwenye jimbo lake. Nimwambie tu, nikitoka hapo tutafanya mawasiliano na DMO wake na uongozi wa wilaya ili tuweze kujua wameweka nini kwenye mpango kwa kushirikiana pamoja na TAMISEMI tuweke huu mkakati wa pamoja wa kuhakikisha hicho kituo kinaenda kujengwa na bajeti ya mwaka ujao.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved