Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Robert Chacha Maboto
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bunda Mjini
Primary Question
MHE. ROBERT C. MABOTO aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Kituo cha Zimamoto katika Halmashauri ya Mji wa Bunda?
Supplementary Question 1
MHE. ROBERT C. MABOTO: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru kwa nafasi. Nina swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Mji wa Bunda au Wilaya ya Bunda ina zaidi ya majimbo matatu ya uchaguzi na ina idadi kubwa sana ya watu. Je, Serikali katika mpango iliyonao katika orodha ya magari ambayo ilisema inayaleta kwa ajili ya zimamoto, Halmashauri ya Mji wa Bunda kwenye orodha hiyo imo?
Name
Geophrey Mizengo Pinda
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kavuu
Answer
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kama ulivyotolewa mwongozo wa orodha ya magari yatakayosambazwa kwenye halmashauri, ninao uhakika Bunda ni moja kati ya Halmashauri zitakazopata magari.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved