Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 46 | Home Affairs | Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi | 588 | 2025-06-16 |
Name
Robert Chacha Maboto
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bunda Mjini
Primary Question
MHE. ROBERT C. MABOTO aliuliza: -
Je, lini Serikali itajenga Kituo cha Zimamoto katika Halmashauri ya Mji wa Bunda?
Name
Innocent Lugha Bashungwa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Karagwe
Answer
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Robert Chacha Maboto, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na jitihada za kusogeza huduma za zimamoto na uokoaji karibu na wananchi kwa kujenga vituo vya zimamoto na uokoaji. Aidha, katika mwaka 2025/2026 Serikali kupitia Jeshi la Zimamoto na Uokoaji imetenga fedha kiasi cha shilingi milioni 400 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Zimamoto na Uokoaji katika Halmashauri ya Mji wa Bunda.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved