Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Daniel Awack Tlemai
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Karatu
Primary Question
MHE. DANIEL A. TLEMAI aliuliza: - Je, lini Serikali itatimiza ahadi yake ya kupeleka Shilingi Bilioni 4.5 Karatu ili wananchi wapate huduma ya uhakika ya maji?
Supplementary Question 1
MHE. DANIEL A. TLEMAI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu ya maswali ya Serikali, nina swali moja la nyongeza.
Je, kwa kuwa ahadi imechukua miaka miwili toka Serikali itoe ahadi, nini mkakati wa Serikali ili kupunguza adha ya upungufu wa maji katika Mji wa Karatu? (Makofi)
Name
Maryprisca Winfred Mahundi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI K.n.y WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, mkakati wa Serikali kuhakikisha Mji wa Karatu unapunguza kadhia ya maji, kwanza mradi huu ambao tayari tumeweka fedha zaidi ya Shilingi Bilioni 1.3 mwaka huu wa fedha 2025/2026 Wizara imetenga Shilingi Milioni 864 kuhakikisha kazi zitaendelea na kadri fedha zinavyopatikana basi tutahakikisha mradi huu unawekewa fedha ili uweze kukamilika.
Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo Serikali itaendelea kuboresha mambo mbalimbali kama uchimbaji wa kisima ambacho kitakuwa zaidi ya mita 200, lengo ni kuhakikisha tunaweza kupata vyanzo vingine vya maji na kuweza kusambaza. Vilevile, visima ambavyo tayari vilichimbwa Wizara itahakikisha inakwenda kuviendeleza kwa kuhakikisha sasa vinasambaza katika maeneo yote yaliyokusudiwa. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved