Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 25 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 326 | 2025-05-15 |
Name
Daniel Awack Tlemai
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Karatu
Primary Question
MHE. DANIEL A. TLEMAI aliuliza: -
Je, lini Serikali itatimiza ahadi yake ya kupeleka Shilingi Bilioni 4.5 Karatu ili wananchi wapate huduma ya uhakika ya maji?
Name
Jumaa Hamidu Aweso
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Pangani
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI K.n.y WAZIRI WA MAJI alijibu: -
Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kutoa fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maji inayolenga kuboresha huduma ya majisafi na salama kwa wananchi wa Karatu Mjini. Katika mwaka wa fedha 2024/2025, jumla ya shilingi 1,371,878.043 zimetolewa kwa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Karatu (KARUWASA) ikiwa ni sehemu ya ahadi ya Serikali ya kuboresha huduma ya maji katika eneo hilo.
Mheshimiwa Spika, fedha hizo zimewezesha kukamilisha utekelezaji wa Mradi wa Maji Ayalabe na kuanza kwa utekelezaji wa Mradi wa Maji Bwawani Na. 3 ambayo kwa pamoja inanufaisha zaidi ya watu 18,880 kwa maeneo hayo.
Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutoa kipaumbele cha kupeleka fedha za utekelezaji wa miradi ya maji katika Jimbo la Karatu kadri fedha zinavyopatikana.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved