Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Conchesta Leonce Rwamlaza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA K.n.y. MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza: - Je, lini ujenzi wa Bwawa la Yongoma - Same utaanza baada ya kukamilika kwa usanifu wa kina?

Supplementary Question 1

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Kwa kuwa kata alizozitaja ambazo ni Maore, Ndungu, Kalemawe, Kihurio na Bendera, zimeathiriwa sana na ukame kutokana na hali ya mabadiliko ya tabia ya nchi na kwa kuwa wananchi wanashughulika na Kilimo. Je mnamkakati wa kumaliza bwawa hilo haraka ili wananchi waweze kufaidika? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, kuna mradi wa BBT katika Wilaya ya Muleba, Kata ya Kamachumu, Kata ya Ruhanga, Kijiji Makongola na mradi huo wananchi wanapanda …. na unaendelea vizuri lakini kuna tatizo kubwa sana la maji ya kumwagilia. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba maji yanapatikana ili mradi huu uweze kuwa na tija. (Makofi)

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusu mpango wa kumaliza mradi huu wa Yongoma kwa haraka? Ndiyo, ni mpango wa Serikali na ndio maana tumeshakamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa kina na tumeweka kwenye bajeti ya mwaka 2025/2026 kwa ajili ya utekelezaji wa bwawa na eneo linalofaa kwa Kilimo.

Mheshimiwa Spika, ni ukweli ukanda ule wakati wa kiangazi, wakati wa masika wanapata maji mengi sana kwa muda mfupi, wakati wa kiangazi wanakuwa na ukame. Kwa hiyo, niwahakikishie tu wananchi wa maeneo hayo kwamba Serikali itaanza kujenga bwawa hili katika Mwaka wa Fedha wa 2025/2026 pamoja na eneo la hekta zaidi ya 1,000 ambazo zitakuwa ni kwa ajili ya Kilimo.

Mheshimiwa Spika, kuhusu mradi wa BBT wa Kagera, kwanza niseme tu niwakupongeze viongozi wa Serikali wa mkoa lakini nitumie nafasi hii kuwahakikishia na wewe mwenyewe Mheshimiwa Mbunge nikushukuru kwa wewe kuwa sehemu ya wakulima wa eneo lile, nakushukuru sana.

Mheshimiwa Spika, nikuhakikishieni tatizo la barabara zile kilometa chache tunaziweka kwenye bajeti ya mwaka kesho na tutawachimbia visima, kwa sababu tayari usanifu umeonyesha kwamba upatikanaji wa maji yapo, tutaleta magari kwa ajili ya uchimbaji kwenye eneo lile. (Makofi)

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA K.n.y. MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza: - Je, lini ujenzi wa Bwawa la Yongoma - Same utaanza baada ya kukamilika kwa usanifu wa kina?

Supplementary Question 2

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kupata nafasi hii, naomba kuuliza swali langu la nyongeza ambalo Mheshimiwa Waziri ni la muhimu sana. Kwa kuwa Bwawa la Yongoma linahitajika sana kwenye kata zilizotajwa hapo. Je, Serikali hamuoni kwamba mchukue ujenzi wa bwawa hili kama mkakati mkubwa wa Serikali? Ahsante. (Makofi)

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mama Kilango, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, yeye mwenyewe alinipeleka tukatembelea Ndungu, tukatembelea hadi kule juu milimani na ameona Serikali imeanza kutekeleza mradi wa Mlimani, tumeanza kutekeleza mradi wa skimu ya Ndungu. Nikuhakikishie Mheshimiwa Mama Kilango na wananchi wa Same, kama tulivyowaahidi kwenye mkutano pale kijijini mimi na wewe, mradi huu tutautekeleza na tutajenga bwawa hili na skimu hii kama inavyotarajiwa. (Makofi)

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA K.n.y. MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza: - Je, lini ujenzi wa Bwawa la Yongoma - Same utaanza baada ya kukamilika kwa usanifu wa kina?

Supplementary Question 3

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kuuliza swali. Je, ni lini sasa Serikali itakamilisha usanifu wa kina katika Bwawa la Magubike katika Kata ya Nzihi?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kiswaga, kama ifuatavyo; -

Mheshimiwa Spika, wataalam wapo hatua za mwisho kumalizia Bwawa la Magubike na nikuahidi Mheshimiwa Kiswaga, kwenye bajeti ya mwaka kesho 2025/2026 Magubike itakuwepo na tutaanza ujenzi.

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA K.n.y. MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza: - Je, lini ujenzi wa Bwawa la Yongoma - Same utaanza baada ya kukamilika kwa usanifu wa kina?

Supplementary Question 4

MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Spika, ahsante. Bwawa la Goeko awamu ya kwanza lipo asilimia 98, tuna awamu ya pili na Mkandarasi ameshapatikana. Ni lini sasa Mkandarasi atakwenda kukabidhiwa site na kuanza ujenzi wa Bwawa la Goeko ambalo katika historia ni bwawa kubwa? (Makofi)

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Venant, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru kwa support anayotoa kwenye mradi wa Goeko kama Mbunge, Mkandarasi ameshapatikana, mkataba umeshasainiwa na sasa tumepeleka maombi Wizara ya Fedha kwa ajili ya kupata advance payment kwa ajili ya yeye kwenda site. Nimuhakikishie tu kwamba mradi ule phase two unahusisha bwawa hilo kulikamilisha na vilevile kujenga jumla ya hekta 3,000 ambazo tulitembelea pamoja mimi na yeye kukagua lile eneo. Nashukuru.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA K.n.y. MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza: - Je, lini ujenzi wa Bwawa la Yongoma - Same utaanza baada ya kukamilika kwa usanifu wa kina?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipatia swali la nyongeza. Ningependa kujua ujenzi wa Bwawa la Kidete utakamilika lini, ili kupunguza maporomoko ya Mto Mkondoa Wilayani Kilosa? Ahsante sana.

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba tu nimwambie Mheshimiwa Ishengoma, kwamba Bwawa la Kidete ni moja ya mabwawa muhimu, kwa maana ya ukanda wa yale mabwawa matano yote, kwa ajili ya kuondoa matatizo ya mafuriko katika Wilaya ya Kilosa na Serikali itaendelea kusukuma kuhakikisha hiyo miradi yote inakamilika kwa wakati.