Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 1961-1995 | Session 1 | Sitting 1 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 324 | 2025-05-15 |
Name
Naghenjwa Livingstone Kaboyoka
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA K.n.y. MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza: -
Je, lini ujenzi wa Bwawa la Yongoma - Same utaanza baada ya kukamilika kwa usanifu wa kina?
Name
Hussein Mohamed Bashe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nzega Mjini
Answer
WAZIRI WA KILIMO alijibu: -
Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kaboyoka, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Spika, Wizara ya Kilimo kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji ilikamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa Bwawa la Yongoma lenye ukubwa wa mita za ujazo 5.8 katika mwaka 2023/2024. Baada ya usanifu kukamilika, mradi huo umewekwa kwenye mpango wa ujenzi kwa mwaka 2025/2026. Kukamilika kwa ujenzi wa bwawa hilo kutawezesha kumwagilia eneo lenye ukubwa wa hekta 1,800 na kunufaisha wakulima 11,150 katika kata za Fidia, Ndungu, Kalemawe na Bendera.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved