Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Mariamu Nassoro Kisangi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. MARIAM N. KISANGI K.n.y MHE. SAADA MANSOUR HUSSEIN aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha matumizi ya mkaa mbadala yanaenezwa hadi Zanzibar?
Supplementary Question 1
MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha kwamba, maeneo yote katika nchi ya Tanzania wanapata nishati hiyo mbadala?
Name
Judith Salvio Kapinga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, ninashukuru kwa swali la nyongeza la Mheshimiwa Mariam Kisangi, ni kweli Serikali inao mkakati kupitia STAMICO, miezi michache iliyopita makontena haya yalisambazwa kwenye mikoa mbalimbali kulingana na zone zake, kwenye ile mikoa ambayo haijafikiwa pia STAMICO wanao mkakati wa kuendelea kupeleka makontena haya ili kuhakikisha mkaa huu wa Rafiki Briquettes unaendelea kutumika katika maeneo yote ya nchi. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, Serikali inao mkakati sasa hivi makontena yamefika kwenye mikoa mingi na tutaendelea hivyo hivyo kwa awamu zinazokuja.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved