Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 17 | Energy and Minerals | Wizara ya Nishati | 215 | 2025-05-05 |
Name
Saada Mansour Hussein
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. MARIAM N. KISANGI K.n.y MHE. SAADA MANSOUR HUSSEIN aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha matumizi ya mkaa mbadala yanaenezwa hadi Zanzibar?
Name
Judith Salvio Kapinga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuhakikisha kwamba, matumizi ya mkaa mbadala yanaenezwa hadi Zanzibar, Serikali kupitia Shirika la Madini (STAMICO) imesajili mawakala wanne kwa ajili ya kuhakikisha mkaa mbadala uitwao Rafiki Briquettes unafika Zanzbar.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mawakala hawa ni Chama cha Ushirika, Maisha Gemu, Salum Omar, Easy Fix na Wanawake na Samia Magharibi B. Aidha, juhudi pia zinafanyika ili kupata eneo ambalo STAMICO wataweka kontena kubwa ambalo litakuwa linapokea mkaa huu mbadala wa Rafiki Briquettes ili kuihifadhi kwa ajili ya kusambazwa katika maeneo yote ya Zanzibar.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved