Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bakar Hamad Bakar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. BAKAR HAMAD BAKAR aliuliza: - Je, lini ahadi ya ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Chakechake itatekelezwa?

Supplementary Question 1

MHE. BAKAR HAMAD BAKAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru sana. Ahadi ya ujenzi wa Kituo hiki cha Wilaya ya Chakechake ni ahadi ya muda mrefu sasa. Ninataka nifahamu ni upi mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba, fedha hizi, shilingi milioni 800, zinapatikana kwa ajili ya kwenda kujenga kituo hiki? Pia, nyumba za Askari na Maafisa mbalimbali wa pale Madungu, Chakechake, ni chakavu na ni za muda mrefu sana.

NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tuko kwenye kipindi cha bajeti. Ninaomba sana muwe watulivu ndani ya Bunge. Swali Waziri halisikii, meza haikusikii, na hata Hansard watashindwa kuandika haya mahojiano ambayo yako ndani.

Mheshimiwa Waziri.

MHE. BAKAR HAMAD BAKAR: Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa ninakwenda kwenye swali la pili.

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli, ahadi hiyo aliyoisema Mheshimiwa Mbunge ni ya muda mrefu, lakini kwanza tuliongeza kituo hicho kwenye mpango, na sasa, kama nilivyojibu kwenye jibu la msingi, tunatenga fedha kwenye mwaka wa fedha 2026/2027 tayari, kwa ajili ya kuanza ujenzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali la pili la uchakavu wa nyumba za Askari, ni kweli nyumba hizo ni chakavu. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwanza tutatuma wataalamu wetu wakafanye tathmini kuhakikisha kwamba, je, tunafanya ukarabati au kujenga upya nyumba hizo? Kwa hiyo, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge, Serikali italifanyia kazi suala hilo. Ahsante sana.