Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 35 | Home Affairs | Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi | 453 | 2025-05-29 |
Name
Bakar Hamad Bakar
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
House of Representatives
Primary Question
MHE. BAKAR HAMAD BAKAR aliuliza: -
Je, lini ahadi ya ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Chakechake itatekelezwa?
Name
Daniel Baran Sillo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Babati Vijijini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Chakechake imetoa kiwanja Na. 61 chenye ukubwa wa mita za mraba 1,429, eneo la vitongoji, kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Polisi, Daraja “B”, cha Wilaya ya Chakechake. Ujenzi wa kituo hicho utagharimu kiasi cha shilingi 802,926,788. Fedha hizo zitatengwa kwenye Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2026/2027, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved