Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Rashid Abdallah Shangazi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mlalo
Primary Question
MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza: - Je, upi mkakati wa kuzitengeneza barabara za Mkoa wa Tanga zilizopo TARURA zilizofunguliwa kwa fedha za tozo na fedha zilizopelekwa Jimboni?
Supplementary Question 1
MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nikupongeze kwa jitihada hizi kubwa za kuifikisha Bajeti ya Barabara za Vijijini kufikia hizo shilingi bilioni 37 kwa Mkoa wa Tanga, lakini nina maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza. Hii programu ya kupeleka lami hasa katika Miji Midogo imekuwa ikienda hasa kwa kusuasua na kujenga kilomita moja ama mbili. Je, Serikali ipo tayari kuongeza fedha ili angalau katika ile Miji Midogo lami iweze kujengwa angalau kwa kiwango cha kilometa tano mpaka 10?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Barabara nyingi ambazo zimefunguliwa vijijini, bado zinahitaji uboreshaji hasa kwa maeneo ya kalavati na pia kujengea sehemu ambazo ni za mifereji hasa katika Wilaya ya Lushoto ambayo maeneo mengi ni ya milima. Je, Serikali ipo tayari sasa kuongeza bajeti katika barabara hizo mpya zilizofunguliwa ili ziweze kupitika kwa mwaka mzima? (Makofi)
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA): Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba nianze kumpongeza Mheshimiwa Rashid Shangazi ambaye amekuwa akifuatilia na kuweka msukumo wa maendeleo katika Jimbo lake.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na swali lake la kwanza ninaomba kumpata taarifa Mheshimiwa Rashid Shangazi kwamba, katika kipindi cha miaka minne ya Serikali Awamu ya Sita, utaona dhamira ya dhati ya kuendelea kuimarisha miundombinu ya barabara zetu hizi za zinazohudumiwa na TARURA za ngazi ya Wilaya.
Mheshimiwa Naibu Spika, zaidi ya shilingi bilioni 100 zimetumika katika Mkoa wa Tanga kwa ajili ya kuimarisha miundombinu ya barabara hizi. Kwa hiyo, ninaomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge hata katika mwaka wa fedha 2025/2026 kwa maana ya mwaka wa bajeti unaofuata tayari fedha inatarajiwa kutumika bajeti imetengwa shilingi bilioni 37.1 kwa ajili ya kwenda kuimarisha miundombinu ya barabara hizi katika Mkoa wa Tanga, ikiwemo katika maeneo ya Miji Midogo ili lami ziweze kujengwa na barabara hizi ziweze kuwanufaisha wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na barabara hizi ambazo zimefunguliwa za vijijini ambazo zinauhitaji wa kalavati, mifereji ikiwemo katika Jimbo la Mheshimiwa Mbunge la Lushoto, ninaomba nimtaarifu kwamba katika bajeti hiyo ya shilingi bilioni 37.3 ya mwaka wa fedha ujao, tayari kuna mipango ambayo ipo ya kujenga kalavati 33, mifereji ya maji kilometa 1,020.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ninaomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, ataona dhamira ya dhati kabisa ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuimarisha miundombinu hii muhimu kabisa ya barabara katika Mkoa wa Tanga na Jimbo lako hili la Lushoto, ndiyo maana utaona Mkoa wa Tanga ulikuwa una bajeti kila mwaka shilingi bilioni 12.4, lakini sasa tunazungumzia mwaka wa fedha 2025/2027, bajeti itakuwa ni shilingi bilioni 37.1. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved