Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 35 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 447 | 2025-05-29 |
Name
Mwanaisha Ng'anzi Ulenge
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza: -
Je, upi mkakati wa kuzitengeneza barabara za Mkoa wa Tanga zilizopo TARURA zilizofunguliwa kwa fedha za tozo na fedha zilizopelekwa Jimboni?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeongeza bajeti Mkoa wa Tanga kutoka shilingi bilioni 12.4 hadi shilingi bilioni 37.1 ambapo kupitia fedha hizi, baadhi ya barabara zimeweza kufunguliwa, kujengwa kutoka changarawe hadi lami, na barabara za udongo kuwa changarawe. Aidha, barabara zilizosajiliwa ndizo zenye uhalali wa kufanyiwa matengenezo kwa kutumia fedha zinazotolewa na Mfuko wa Barabara.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeongeza barabara za lami kutoka kilomita 124.078 hadi kilomita 165.68 na kuongeza barabara za changarawe kilomita 2,104.25, ambapo kati ya hizo zipo ambazo zilikuwa zimesajiliwa na zinaendelea kufanyiwa matengenezo kwa kutumia fedha kutoka Mfuko wa Barabara.
Mheshimiwa Naibu Spika, hadi sasa, takribani kilomita 1,486.4 za barabara ambazo hazijasajiliwa, tayari Serikali imeshaanza mchakato wa kuzisajili ili zitambulike na kuweza kutengewa fedha kwa ajili ya matengenezo ya mara kwa mara (Routine Maintenance) kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kuihudumia miundombinu ya barabara na madaraja ya Mkoa wa Tanga kwa kujenga, kukarabati na kutengeneza kulingana na upatikanaji wa fedha. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved