Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 16 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) | 181 | 2026-04-24 |
Name
Omary Marcus Msigwa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Madaba
Primary Question
MHE. OMARY M. MSIGWA aliuliza: -
Je, lini Serikali itaongeza Watumishi wa Sekta ya Afya wakiwemo Wataalamu wa Mionzi katika Jimbo la Madaba?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Omary Marcus Msigwa, Mbunge wa Jimbo la Madaba kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kutenga bajeti na kuajiri watumishi wa kada mbalimbali za afya nchini. Katika kipindi cha mwaka 2020/2021 hadi 2025/2026 jumla ya watumishi wa kada mbalimbali za afya 37,921 wameajiriwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka 2025/2026 Serikali imeajiri jumla ya wataalam wa kada mbalimbali za afya 5,000 na kuwapanga katika halmashauri zenye upungufu ikiwemo Halmashauri ya Wilaya ya Madaba iliyopangiwa watumishi 84.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kuboresha miundombinu na huduma katika vituo vya afya ngazi ya msingi hali iliyopelekea mahitaji ya wataalam wa kada za afya ikiwemo wataalam wa mionzi kuongezeka ambapo wanaohitajika ni 1,159 na kwa sasa wapo 338 sawa na 29%.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kuajiri wataalam wa mionzi pamoja na kuwaendeleza wataalam wa kada nyingine 56 wakiwemo watumishi wawili kutoka Halmashauri ya Madaba wanaopata mafunzo ya muda mfupi ya mionzi katika Chuo cha Afya Hydom.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved