Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 16 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) 180 2026-04-24

Name

Salum Khamis Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. THOMAS K. MAGANGA K.n.y. MHE. SALUM K. SALUM aliuliza: -

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Soko la Mnada wa Mifugo ili kuwa na Soko lenye hadhi na kuongeza mapato ya Halmashauri katika Jimbo la Meatu?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Salum Khamis Salum, Mbunge wa Jimbo la Meatu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Meatu inayo minada ya awali minne ya Bukundi, Itinje, Mwanhuzi na Tindabuligi ambayo inahitaji kuboreshwa ili kuweka mazingira mazuri ya kuuza na kununua mifugo katika wilaya hiyo.

Mheshimiwa Spika, kwa kutambua umuhimu huo, katika mwaka wa fedha 2023/2024, Halmashauri ya Wilaya ya Meatu kupitia mapato ya ndani ilitoa shilingi milioni 14.3 kwa ajili ya kuboresha minada hiyo kwa kujenga machinjio, choo na kutwaa eneo la kujenga mnada wa kisasa lenye ukubwa wa ekari nane katika Kijiji cha Bukundi.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2025/2026 Halmashauri imetenga shilingi milioni 12 kwa ajili ya kuanza awamu ya kwanza ya ujenzi wa uzio wa mnada katika eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa mnada wa kisasa wakati taratibu za kutafuta fedha za ujenzi wa mnada huo zikiendelea. Ujenzi wa uzio huo unatarajiwa kuanza Mei, 2026.

Mheshimiwa Spika, ninaomba kuwasilisha.