Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 24 | Justice and Constitutional Affairs | Wizara ya Katiba na Sheria | 276 | 2026-05-07 |
Name
Zacharia Paulo Issaay
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mbulu Mjini
Primary Question
MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: -
Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa jengo la Mahakama ya Wilaya ya Mbulu ambao umesimama kwa muda mrefu?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kwa kushirikiana na Mahakama ya Tanzania imeendelea kutekeleza Mpango wa Ujenzi na Ukarabati wa majengo ya Mahakama kwa lengo la kuimarisha miundombinu ya utoaji haki katika ngazi mbalimbali. Mpango huu unahusisha ujenzi wa majengo mapya pamoja na ukarabati wa majengo yaliyopo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika utekelezaji wa mpango huo, ujenzi wa jengo la Mahakama ya Wilaya ya Mbulu ulianza katika mwaka wa fedha 2024/2025. Hata hivyo, mradi huo umechelewa kukamilika kutokana na changamoto mbalimbali zilizojitokeza wakati wa utekelezaji wake. Tayari changamoto hizo zimetatuliwa na ujenzi wa jengo hilo unaendelea na unatarajiwa kukamilika ifikapo Novemba, 2026.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved