Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 24 | Energy and Minerals | Wizara ya Madini | 274 | 2026-05-07 |
Name
Mwanahamis Athumani Munkunda
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. MWANAHAMISI A. MUNKUNDA aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha Kituo cha Umahiri eneo la Mwakitolyo kutokana na ushiriki mkubwa wa wachimbaji wa madini wanawake na vijana?
Name
Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Longido
Answer
NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Madini, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwanahamisi Athumani Munkunda, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la Mwakitolyo ni moja ya maeneo ambayo Serikali kupitia Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) inapanga kujenga vituo vya mfano vya uchenjuaji madini ya dhahabu kwa kutumia teknolojia ya Carbon-in-Pulp (CIP) kwa mwaka wa fedha 2026/2027. Ujenzi wa vituo hivi ambavyo vingine viko Mikoa ya Geita, Mbeya na Mara ni sehemu ya juhudi za Serikali za kuwaendeleza na kuwakuza wachimbaji wadogo nchini kupitia Shirika la STAMICO.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkandarasi wa kujenga Kituo cha Mwakitolyo ameshapatikana, na taratibu za kimkataba zikikamilika, ujenzi utaanza. Hatua ilivyofikiwa hadi sasa ni kukamilika kwa usanifu wa kituo, na kituo hicho kitakapokamilika, kitakuwa na uwezo wa kuchakata kiasi cha tani 120 kwa siku.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved