Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 24 | Natural Resources and Tourism | Wizara ya Maliasili na Utalii | 273 | 2026-05-07 |
Name
Kangi Alphaxard Lugola
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mwibara
Primary Question
MHE. KANGI A. LUGOLA aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kudhibiti kero ya mamba wanaodhuru wananchi katika Jimbo la Mwibara?
Name
Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Kondoa
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO K.n.y. WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Kangi Alphaxard Lugola, Mbunge wa Jimbo la Mwibara, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imechukua hatua mbalimbali za kudhibiti mamba katika Jimbo la Mwibara ambapo katika mwaka wa fedha 2024/2025, Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia TAWA ilijenga jumla ya vizimba vinne vya kuzuia mamba katika vijiji vya Buzimbwe, Kasahunga, Nampangala na Nyarugoma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia, katika mwaka wa fedha 2025/2026 Wizara inaendelea na ujenzi wa vizimba viwili katika vijiji vya Nyamitwebili na Namibu. Aidha, kwa kuwa changamoto hii haiwezi kwisha kwa mara moja, Wizara kupitia Taasisi ya TAWA itaendelea kujenga vizimba kwenye maeneo yenye changamoto za mamba kudhuru watu kwenye Ziwa Victoria katika Wilaya za Jimbo la Mwibara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile, Wizara imekuwa ikitoa elimu kwa wananchi wa Jimbo la Mwibara ambapo kati ya Mwezi Julai, 2025 hadi Machi, 2026, jumla ya mikutano 12 ilifanyika. Katika mikutano hiyo, wananchi 3,665 ikijumuisha watu wazima 904 na wanafunzi 2,761 walipatiwa elimu ya namna bora ya kutumia vizimba na kuepuka madhara yanayoweza kusababishwa na mamba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, ili kuongeza wigo wa kutoa elimu kwa wananchi, Wizara ilitoa elimu kwa njia ya redio na televisheni ambapo jumla ya vipindi vitano vya redio na televisheni vitatu vilitolewa. Vipindi hivyo, vilitolewa katika redio za Bunda FM na Redio Mazingira, na televisheni ya Star TV ambazo zinasikika zaidi katika Kanda ya Ziwa ikiwemo Jimbo la Mwibara.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved