Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 24 | Natural Resources and Tourism | Wizara ya Maliasili na Utalii | 272 | 2026-05-07 |
Name
Jamal Ramadhan Mwinyi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bumbwini
Primary Question
MHE. MWINYI JAMAL RAMADHAN aliuliza: -
Je, ni wanyama gani wana vibali vya kuwindwa kwa matumizi ya kijamii kwa kuwa nchi yetu ina wanyama wengi katika mapori ya vijijini?
Name
Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Kondoa
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO K.n.y. WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Mwinyi Jamal Ramadhan, Mbunge wa Bumbwini, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, uwindaji kwa matumizi ya kijamii kwa maana ya uwindaji wa kujikimu wa wenyeji, ni moja ya matumizi endelevu ya uvunaji wanyamapori kwa lengo la kutoa fursa kwa wananchi wazawa na wakazi kujipatia kitoweo. Ili kuwezesha wananchi kutumia fursa hiyo, Serikali imetunga Kanuni za Uwindaji wa Kujikimu wa wenyeji za Mwaka 2022 katika Tangazo la Serikali Na. 635 la Mwaka 2022 ambazo zimeainisha taratibu za kufuata ili kuweza kufanya shughuli hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kanuni hizo zimebainisha jumla ya aina 23 ya jamii za wanyamapori ambao wanaruhusiwa kuwindwa kupitia uwindaji wa wenyeji ambapo kati yao jamii ya mamalia zipo 18 wakiwemo nyati, pofu dume ama mbunju, pongo, digidigi, nyumbu na jamii za ndege aina tano wakiwemo bata, kanga na firigogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara inatambua umuhimu wa wananchi kunufaika na rasilimali za wanyamapori, kwani wao ndio walinzi namba moja wa misitu na wanyamapori wetu. Hivyo, Serikali inawaomba wananchi kuzingatia sheria na kanuni zilizopo katika kuwawinda wanyamapori kwa matumizi ya kijamii.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved