Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 24 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 271 2026-05-07

Name

Morris Joseph Makoi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. MORRIS J. MAKOI aliuliza: -

Je, lini Serikali itamrejesha mkandarasi wa barabara ya Moshi International School - Kibosho kwa Rafael yenye urefu wa kilometa 5.49?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Morris Joseph Makoi, Mbunge wa Moshi Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Moshi International School – Kibosho kwa Rafael, kilometa 7.19, ni sehemu ya barabara ya Kibosho Shine – Kwa Rafael – International School yenye urefu wa kilometa 25.25 ambapo kilometa 18.06 tayari zimejengwa kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Serikali imesaini mkataba kwa ajili ya kazi ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa kilometa 7.19 zilizobaki ambapo taratibu za malipo ya awali kwa mkandarasi zinaendelea ili aweze kuendelea na kazi kwa mujibu wa mkataba, ahsante.