Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 24 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 271 | 2026-05-07 |
Name
Morris Joseph Makoi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Moshi Mjini
Primary Question
MHE. MORRIS J. MAKOI aliuliza: -
Je, lini Serikali itamrejesha mkandarasi wa barabara ya Moshi International School - Kibosho kwa Rafael yenye urefu wa kilometa 5.49?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Morris Joseph Makoi, Mbunge wa Moshi Vijijini, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Moshi International School – Kibosho kwa Rafael, kilometa 7.19, ni sehemu ya barabara ya Kibosho Shine – Kwa Rafael – International School yenye urefu wa kilometa 25.25 ambapo kilometa 18.06 tayari zimejengwa kwa kiwango cha lami.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Serikali imesaini mkataba kwa ajili ya kazi ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa kilometa 7.19 zilizobaki ambapo taratibu za malipo ya awali kwa mkandarasi zinaendelea ili aweze kuendelea na kazi kwa mujibu wa mkataba, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved