Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 11 | Home Affairs | Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi | 122 | 2026-04-17 |
Name
Ado Shaibu Ado
Sex
Male
Party
ACT
Constituent
Tunduru Kaskazini
Primary Question
MHE. ADO S. ADO aliuliza: -
Je, lini Serikali itajenga jengo jipya la Magereza Tunduru kwa kuwa jengo lililopo haliendani na mahitaji ya sasa?
Name
Mohammed Mahmoud Ayoub
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Chaani
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Ado Shaibu Ado kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua hali ya uchakavu wa majengo katika magereza mengi hapa nchini likiwemo Gereza la Tunduru. Kwa sasa Serikali kupitia Jeshi la Magereza ina mpango wa ukarabati na upanuzi wa gereza hilo kwa awamu, ambapo tathmini ya uchakavu pamoja na michoro imekamilika na inatarajiwa kugharimu kiasi cha shilingi milioni 465 katika ukarabati na upanuzi huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Jeshi la Magereza itaendelea kutenga fedha kwenye bajeti kila mwaka pamoja na kutumia vyanzo vya ndani vya ubunifu ili kuhakikisha inatekeleza mpango mkakati wa ukarabati na ujenzi wa magereza nchini likiwemo Gereza la Tunduru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuwasilisha.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved