Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 11 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 122 2026-04-17

Name

Ado Shaibu Ado

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. ADO S. ADO aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga jengo jipya la Magereza Tunduru kwa kuwa jengo lililopo haliendani na mahitaji ya sasa?

Name

Mohammed Mahmoud Ayoub

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chaani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Ado Shaibu Ado kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua hali ya uchakavu wa majengo katika magereza mengi hapa nchini likiwemo Gereza la Tunduru. Kwa sasa Serikali kupitia Jeshi la Magereza ina mpango wa ukarabati na upanuzi wa gereza hilo kwa awamu, ambapo tathmini ya uchakavu pamoja na michoro imekamilika na inatarajiwa kugharimu kiasi cha shilingi milioni 465 katika ukarabati na upanuzi huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Jeshi la Magereza itaendelea kutenga fedha kwenye bajeti kila mwaka pamoja na kutumia vyanzo vya ndani vya ubunifu ili kuhakikisha inatekeleza mpango mkakati wa ukarabati na ujenzi wa magereza nchini likiwemo Gereza la Tunduru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuwasilisha.