Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 24 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 270 2026-05-07

Name

Onesmo Merdson Mnkondya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. ONESMO M. MNKONDYA aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga chuo kikuu katika Mkoa wa Songwe?

Name

Wanu Hafidh Ameir

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Onesmo Merdson Mnkondya, Mbunge wa Mbozi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuongeza fursa za upatikanaji wa Elimu ya Juu na kuchochea maendeleo ya kiuchumi, Serikali inaendelea na kukamilisha ujenzi wa kampasi za taasisi za elimu ya juu katika maeneo mbalimbali nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Songwe una taasisi za Elimu ya Juu ikiwemo Kampasi ya Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) ambayo kupitia mradi wa Technical Education Labour Market Survey, Serikali inafanya upanuzi wa miundombinu. Upanuzi huu unahusisha ujenzi wa jengo la ghorofa nne la taaluma ambalo litakuwa na madarasa, maabara pamoja na karakana. Lengo ni kuongeza udahili wa wanafunzi katika fani mbalimbali kuanzia ngazi ya cheti hadi degree.