Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 24 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) | 269 | 2026-05-07 |
Name
Kenneth Ernest Nollo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bahi
Primary Question
MHE. ESTER A. BULAYA K.n.y. MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza: -
Je, lini Serikali itatimiza ahadi ya ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Mtitaa Bahi?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Kenneth Esnest Nollo, Mbunge wa Jimbo la Bahi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kituo cha Afya Mtitaa kilichopo katika Kata ya Mtitaa Halmashauri ya Bahi ni miongoni mwa vituo vya afya kongwe 205 ambavyo Serikali imevianzisha kwa ajili ya ukarabati na kuviongezea miundombinu ili viweze kutoa huduma ya afya ngazi ya kituo cha afya, ikiwemo huduma ya upasuaji wa dharura kwa wajawazito.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2024/2025 Serikali kupitia Mradi wa Benki ya Dunia wa Usafi na Afya ya Mazingira (WASH) ilitoa shilingi milioni 73.83 kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu ya majisafi na majitaka pamoja na ujenzi wa choo cha nje kwa ajili ya wagonjwa katika Kituo cha Afya cha Mtitaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ukarabati na ujenzi wa miundombinu ya vituo vya afya kongwe kote nchini. Aidha, katika mwaka wa fedha 2026/2027 Serikali imetenga shilingi milioni 130 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa Kituo cha Afya Babayu katika Halmashauri ya Wilaya ya Bahi.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved