Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 11 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 126 | 2026-04-17 |
Name
Nuru Issa Kashakari
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kigoma Kusini
Primary Question
MHE. NURU I. KASHAKARI aliuliza: -
Je, lini Serikali itajenga Daraja la Mto Malagarasi, Kijiji cha Ilagara ili kuwasaidia wananchi wa ukanda wa Ziwa Tanganyika?
Name
Abdallah Hamis Ulega
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mkuranga
Answer
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI K.n.y. WAZIRI WA UJENZI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Nuru Issa Kashakari, Mbunge wa Kigoma Kusini, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekamilisha kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi wa Daraja la Mto Malagarasi lililopo Kijiji cha Ilagala katika Barabara ya Simbo – Kalya (kilometa 231.29). Kwa sasa, Serikali inatafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa daraja hilo.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved