Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 11 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 126 2026-04-17

Name

Nuru Issa Kashakari

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. NURU I. KASHAKARI aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga Daraja la Mto Malagarasi, Kijiji cha Ilagara ili kuwasaidia wananchi wa ukanda wa Ziwa Tanganyika?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI K.n.y. WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Nuru Issa Kashakari, Mbunge wa Kigoma Kusini, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekamilisha kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi wa Daraja la Mto Malagarasi lililopo Kijiji cha Ilagala katika Barabara ya Simbo – Kalya (kilometa 231.29). Kwa sasa, Serikali inatafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa daraja hilo.