Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 11 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 125 2026-04-17

Name

Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KUNTI Y. MAJALA aliuliza: -

Je, lini ujenzi wa barabara kutoka Handeni kupitia Olboloti - Mrijo - Chemba - Kwamtoro hadi Singida utaanza?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI K.n.y. WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Kunti Yusuph Majala kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeanza ujenzi wa Barabara ya Handeni – Kibirashi – Kiteto – Mrijo – Chemba hadi Singida yenye urefu wa kilometa 424.24 kwa awamu, ambapo kwa sehemu ya kwanza ya kutoka Handeni – Mafuleta (kilometa 20) ujenzi umefikia 52.6%.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, sehemu ya pili ya Mafuleta – Kileguru (kilometa 30) na Kibaya – Kisima (kilometa 50) wakandarasi wapo kwenye maandalizi ya kuanza ujenzi. Kwa sehemu iliyobaki, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) na Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) wako kwenye majadiliano ya awali ya kuijenga kwa utaratibu wa PPP.